|
Rais
wa Zanzibar Mhe.Dkt.Ally Mohamed Shein akisalimiana na Mhe. Dkt.
Harrison Mwakyembe Waziri wa Katiba na Sheria mara baada ya kuwasili
katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro kwaajili ya
kuhudhuria Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa umoja wa Afrika
Mashariki
|
|
Rais Mhe. Dkt. Ally Mohamed Shein akivipongeza vikundi vya wacheza ngoma vilivyokuja kumpokea uwanjani hapo. |
|
Kikundi cha ngoma cha wanawake kikimpokea kwa shangwe Mhe. Rais wa Zanzibar.
|
|
Rais
wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro kwaajili ya kuhudhuria
Mkutano wa 17 wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,
Mhe. Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe wa pili kulia
aliongoza mapokezi ya kiongozi huyo.
|
|
Rais
wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akisalimiana na viongozi wa jeshi ambao
walikuja kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro,
kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Charles Kitwanga akiwa
ameambatana naye mara baada ya kumpokea.
|
|
Kaimu
Mkuu wa Itifaki Bw. James Bwana akitoa maelekezo kwa Mhe. Waziri wa
Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo ambaye alimpokea Rais wa Kenya
Mhe. Uhuru Kenyata ambaye aliwasili kwaajili ya kushiriki mkutano huo.
|
|
Rais
wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyata akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini
Kenya Mhe.John Haule mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Kilimanjaro. |
|
Mhe, Rais Uhuru Kenyata akisalimia vikundi vya ngoma havipo pichani vilivyokuwa vikitoa burudani uwanjani hapo.
Wakuu
wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika
Mkutano wa 17 ambapo katika Mkutano huo Sudan ya kusini nayo imepata
usajili wa uanachama katika umoja huo baada ya maombi yake kujadiliwa na
kukubaliwa.
|
Mhe
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni mwenyekiti wa jumuiya hiyo
akihutubia katika Mkutano, ambapo ilikuwa mara yake ya kwanza kushiriki
Mkutano huo tangu ashinde uchaguzi na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania.
|
|
Katibu
Mkuu mteule wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Bw, Liberat Mphumukeko
kutoka nchini Burundi akiapa katika mkutano huo wa wakuu wa nchi mara
baada ya uteuzi wake.
|
Bw.
Liberat Mphumukeko akipewa pongezi na Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje,
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa nchini
Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga mara baada ya kukamilisha
taratibu za kiapo.
|
Waheshimiwa
marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa wameshika Hati ya
kimataifa ya kusafiria ndani ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo ambapo
uzinduzi wa hati hiyo ulifanyika katika mkutano huo.
|
|
Kijana
Simon Moleli kutoka shule ya Sekondari ya Mzumbe ambaye alikuwa mshindi
wa kwanza katika mashindano ya uandishi wa insha ya Afrika Mashariki
mara baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi na fedha vikiwa ni tuzo kwa
ushindi alioupata.
|
|
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Balozi Innocent Shio wa pili kutoka kushoto akifatilia mkutano.
|
|
|
|
This post was written by: Author Name
Your description comes here!
Get Free Email Updates to your Inbox!
Filed Under:
EAC
on Thursday, March 3, 2016
Post a Comment