BODI
ya Utalii Tanzania (TTB) imekanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao
kuhusu eneo la Olduvai Gorge kuwepo nchini Kenya, ikisisitiza kuwa eneo hilo
lipo Tanzania.
Taarifa
kwa vyombo vya habari iliyotolewa na TTB Dar es Salaam jana ilisema kuwa
taasisi hiyo imekuwa ikifuatilia video iliyotumwa katika YouTube https://www.youtube.com/watch?=iveX49WE7fw na
imekuwa ikisambazwa kupitia njia mbalimbali za habari ikimuonesha mtu mmoja
kutoka nchi jirani akisema kuwa Olduvai Gorge ambayo kimsingi iko Tanzania
kwamba iko Kenya.
Ilisema
kimsingi eneo hilo la Olduvai Gorge liko katika Bonde la Ufa katikati ya Bonde
la Ngorongoro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Manyara nchini Tanzania.
Ilisema
Video hiyo imeibua majadiliano katika mitandao ya kijamii baina ya watanzania
na watu wengine ambao wanaitakia mema Tanzania na wanaoelewa vizuri kuwa
Olduvai Gorge iko Tanzania.
Taarifa
ilibainisha kuwa TTB kama taasisi ya Umma yenye jukumu la kuvitangaza vivutio
vya utalii imeshtushwa na video hiyo iliyojaa upotoshwaji ambao wanaamini mbali
ya malengo mengine ililenga kuchafua kazi nzuri inayofanywa na TTB kwa
kushirikiana na wadau wengine katika kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania
ikiwemo Olduvai Gorge.
Iliongeza
kuwa TTB inapinga vikali upotoshwaji huo uliofanywa na mtu huyo wakati
akihutubia mkutano ambao ulikuwa ni wa Vijana wa Umoja wa Mataifa uliofanyika
Amerika mwezi Agosti mwaka jana.
Ilifafanua
kuwa TTB inapenda dunia ifahamu kuwa kama ilivyo kwa Mlima Kilimanjaro, Hifadhi
ya Taifa ya Serengeti, Zanzibar na nyinginezo, Olduvai Gorge mahali
panapoaminika kuwa ndipo binadamu wa kwanza duniani aliishi na ambako Dr. Louis
na Mary Leakey waligundua fuvu la binadamu huyo wa kale anayesadikiwa kuishi
miaka takribani milioni 2 iliyopita iko pia Tanzania na si mahali pengine
popote duniani.
TTB
inatoa wito kwa watanzania kuendelea kuunga mkono juhudi zao za kuvitangaza
vivutio vya Utalii kwa kujibu na kusahihisha papo hapo upotoshaji kuhusu
Tanzania unapotokea ndani ya nchi au nje.
Mwisho.
Post a Comment