Mwimbaji
anaekuja kwa kasi kwenye muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva) kutoka Tanzania
anayewakilisha kundi la Wasafi Classic Baby(Wcb),Harmonize ameachia
wimbo wake wimbo mpya unaoitwa ‘BADO’ aliyomshirikisha Diamond Platnumz.
SABABU
YA KUREKODI WIMBO HUU.
Kwa
singo mbili alizosikika Harmonize(Aiyola,Kidonda Changu) kwenye vyombo vya
habari,jamii imekua ikimfananisha sana na Diamond kwenye uimbaji,ndipo siku moja
Harmonize wakati akiimba Diamond alivutiwa na Melody ya wimbo huu na kusema hii
itakua nafasi ya Watanzania kuwatofautisha kwenye uimbaji.
KUHUSU
WIMBO WA BADO.
Harmonize
alikaa na Diamond akamuuliza ni msichana gani alishamuumiza kiasi kwamba hawezi
kumsahau,ingawa Diamond hakumwambia ni msichana gani,lakini akamwambia hiyo ni
idea(Mwanga) mzuri wa kutunga wimbo ‘mkali’ Beat ya wimbo huu imetengenezwa na
Mtayarishaji(Producer) anaitwa Fraga na kabla ya kurekodi kwenye studio ya
Wasafi,producer Fraga alimtumia midundo (Beat) 3 Harmonize achague,ndipo
akachagua beat ya wimbo huu na kurudi Wasafi Records kwa ajili ya kurekebishwa
na kuanza kurekodiwa.
VIDEO
YA WIMBO WA BADO.
Video ya wimbo huu imefanyika Afrika Kusini
na Muongozaji(Director) anaitwa Nick ambaye ametengeneza video kadhaa ikiwemo
Aiyola ya Harmonize mwenyewe,Make Me Sing ya Aka na Diamond,Love Boat Kcee
na.Diamond,Walk it off ya Fid Q na nyingine nyingi
Post a Comment