|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
akiwasalimia wakazi wa Arusha, viongozi na wawakilishi wa mataifa
mbalimbali hawapo pichani ambao walihudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa
ujenzi wa mradi wa barabara ya Arusha -Holili/Taveta -Voi km 234.3
uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha, tarehe 3 March,2016.
|
Waziri
wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Masharika, Kikanda na Kimataifa
na Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Augustine
Mahiga akiwasilisha taarifa ya Tanzania katika hafla ya uzinduzi wa
ujenzi wa mradi wa barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km234.3.
|
|
|
Mhe.
Rais Dkt. Magufuli na Mhe. Rais Uhuru Kenyata wakiongoza zoezi maalum
la kukata utepe kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa Mradi wa barabara
Arusha-Holili/Taveta-Voi, wakiwa pamoja na wakuu wa nchi za Jumuiya ya
Afrika Mashariki na viongozi mbalimbali walioshiriki hafla fupi ya
Uzinduzi huo.
|
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Magufuli na Mkurugenzi wa
Benki ya Maendeleo ya Afrika (Nairobi) Gabriel Negata wakimwagilia maji
mti mara baada ya zoezi la uzinduzi wa barabara.
|
|
Mhe.
Rais akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa nchi wa wananchama wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki na viongozi wawakilishi wa mataifa
mbalimbali walioshiriki uzinduzi huo.
|
|
Rais
wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akiagana na Mhe. Waziri wa Katiba
na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe tayari kwa kuanza safari ya kurudi
nchini Uganda mara baada ya kukamilisha shughuli zilizoambatana na
Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
|
|
Rais
wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyata akitoa neno la shukuran kwa waziri wa
Nishati na Madini Mhe. Sospeter Muhungo kuishukuru Serikali ya Tanzania
tayari kwa safari ya kurudi nchini Kenya mara baada ya kukamilisha
ushiriki wa Mkutano na kuzindua mradi wa ujenzi wa barabara
unayoiunganisha nchi ya Kenya na Tanzania.
|
|
Rais
wa Zanzibar Mhe. Dkt. Ally Mohamed Shein akiondoka katika uwanja wa
Kimataifa wa Kilimanjaro kwa safari ya kuelekea visiwani Zanzibar mara
baada ya kukamilisha zoezi la uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya
Arusha -Holili/Taveta-Voi uliofanyika Tengeru nje kidogo ya Jiji la
Arusha, tarehe 3 Machi,2016.
|
This post was written by: Author Name
Your description comes here!
Get Free Email Updates to your Inbox!
Filed Under:
EAC
on Friday, March 4, 2016
Post a Comment