Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MFUKO WA PENSHENI WA PPF KUTOA HUDUMA ZOTE KWA WATEJA WAKE VIWANJA VYA SABASABA

Muonekano wa nje ya Jengo la PPF lililopo Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa vya Mwalimu Nyerere jijini Dar esSalaam (Sabasaba). Maandalizi. Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally (katikati) na Afisa Michango Glory Maboya, wakijiandaa kuhudumia wateja leo asubuhi katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba. Afisa Utafiti Neema Mjema (nyuma) na Mwanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nyambilila Ndoboka, pia wakijiandaa kuweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Bandao lao la Maonesho kwenye Viwanja vya Sabasaba leo. Afisa Uwekezaji wa Mfuko huo, Jonas Mbwambo akiweka mambo sawa kabla ya kuanza kupokea wateja katika Banda lao namba 86 viwanja vya Saba saba. Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Pauline Msanga, akitoa maelezo kwa wananchi kuhusu Huduma za uendeshaji Mfuko huo, wakati walipotembelea katika Banda lao lililopo kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, leo. Sehemu ya wananchi waliotembelea Banda la Mfuko wa Pensheni wa PPF wakipata elimu kuhusu Mafao yatolewayo na Mfuko huo na jinsi mwanachama anavyoweza kujiunga na kuchangia. Afisa Michango wa Mfuko huo, Saluna Aziz Ally, akimfafanulia mwanachama wake kuhusu uchangiaji wa michango ya Wanachama, Afisa Huduma kwa Wateja wa PPF, Mwajuma Msina, akizungumza na Mwananchi aliyefika kutembelea Banda hilo wakati akimwelezea kuhusu huduma zinazotolewa na Mfuko huo. Afisa Mafao wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Tulla Mwigune (kulia) akifafanua jambo kwa mstaafu wa PPF. Mtaalamu wa Mifumo ya Habari wa Mfuko wa PPF, Isabela Ngalawa, akimwelekeza mmoja kati ya Wanachama wa Mfuko huo kuhusu 'PPF Taarifa Mobile Apps' ili mwanachama aweze kupata taarifa za michango yake kupitia simu yake ya mkononi. Afisa Huduma kwa Wateja, Mohamed Siaga, akizungumza na Mwananchi aliyefika katika Banda la PPF kuhusu jinsi ya kujiunga na Mfumo wa 'Wote scheme kutoka sekta isiyo rasmi. Mmoja kati ya Wanasheria wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nyambilila Ndoboka, akimwelekeza jambo mwanachama wa Mfuko huo kuhusu masuala ya Kisheria, wakati alipofika kutembelea Banda la Maonesho la PFF leo. Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Temeke, Sostenes Lyimo (kushoto) akifafanua jambo kwa baadhi ya wananchi waliotembelea Banda hilo. Baadhi ya Wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya Banda lao Namba 86 lililopo katika Viwanja vya Sabasaba.
Picha Zote na Mafoto Blog
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top