Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

JERRY MURO AFUNGUKA BAADA YA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA(TFF) KUMFUNGIA KWA MWAKA MMOJA

Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Yanga Jerry Muro jioni ya July 7 2016 ameingia kwenye headlines baada ya shirikisho la soka Tanzania TFF kupitia kamati ya maadili, kutangaza kumfungia mwaka mmoja kujihusisha na soka na faini ya Tsh milioni 3.

Jerry Muro amefungiwa na kamati ya maadili kwa makosa mawili, moja alilifanya mwaka 2015 la kukaidi kulipa faini ya Tsh milioni 5 iliyoamuliwa kulipa na kamati ya nidhamu baada ya kufanya makosa, kosa ambalo limemfanya afungiwe mwaka mmoja kujihusisha na soka.


Kosa la pili ni kutuhumiwa kuchochea vurugu kuelekea mchezo wa Yanga wa Kombe la shirikisho dhidi ya TP Mazembe uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam, baada ya hukumu hiyo Jerry Muro ameongea haya:

“Taarifa hizo nimezisikia japo kwa sasa nipo kijijini Machame kwa ajili ya likizo yangu, nimesikia watu wameandika kwenye mitandao kuwa nimefungiwa, lakini mimi nipo Machame na maamuzi yao yametoka nikiwa likizo Machame, yaani wametoa hukumu kwa kusikiliza upande mmoja”
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top