Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KUELEKEA SEPTEMBA MOSI POLISI WAENDELEA NA MAZOEZI HUKO MOSHI

Moshi. Mazoezi ya Polisi mkoani Kilimajaro yaliyodumu kwa takriban saa nne yaliyofanywa na vikosi vya askari wa kutuliza ghasia na magari ya washawasha, yametikisa mji wa Moshi na kuzua hofu kwa  wananchi.
Baadhi ya wananchi walishangazwa na kitendo hicho cha polisi  kuzunguka wakiwa na mabomu ya machozi na gari la maji ya washawasha.

Mkazi mmoja, Peter Lyimo alisema ameshtushwa kuona magari ya polisi yakizunguka, huku milio ya milipuko ya mabomu ikisikika.

Naye Mary Kavishe alisema: “Tumezoea kuona polisi wakifanya mazoezi kambini kwao, siyo kuzunguka katikati ya mji.”

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbrod Mutafungwa  alisema wanafanya mazoezi ya kawaida ya kujihami na wahalifu  na kulinda wananchi na mali zao.

“Ni mazoezi ya kawaida na yanafanyika mkoa mzima kwa ajili ya kuimarisha askari wetu,  ili kujihami na matukio mbalimbali ya kihalifu,” alisema.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top