Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Helkopta ya uchaguzi yashambuliwa Libya


Watu wenye silaha wemeishambulia helikopta iliyokuwa ikibeba
vifaa vya uchaguzi vitakavyotumika kwa ajili ya kupiga kura katika uchaguzi wa
Jumamosi nchini Libya, maafisa wa nchi hiyo wamesema.
Helikopta hiyo ililazimishwa kutua nje ya mji wa mashariki wa Benghazi.
Taarifa ambazo hazijathitishwa zinasema mtu mmoja amefariki.
Utambulisho wa washambuliaji bado haujajulikana, lakini eneo la mashariki mwa
Libya limekosa utulivu kutokana na makundi yanayotafuta uhuru wa kanda hiyo.
Uchaguzi wa wabunge ni za kwanza nchini humo baada Marehemu Muammar Gaddafi
kupinduliwa mwaka jana.
Habari hizi zinakuja wakati watu wenye silaha wamefunga vituo vitatu vya
kuuza nje mafuta kupinga uchaguzi huo.
Watu hao wamekasirishwa kwamba eneo la magharibi ya nchi limepewa viti 200
zaidi katika Bunge jipya ikilingalishwa na eneo la mashariki lenye utajiri wa
mafuta.
Kulingana na shirika la habari la Reuters, nusu ya vituo vya Libya vya kuuza
nje mafuta vimefungwa kutokana na hali hiyo.
"Helikopta iliyobeba masanduku ya kura iliruka juu eneo la Hawari Kusini mwa
Benghazi ambapo alipigwa kwa kuwa kutumia silaha ndogo," AFP limenukuu shirika
la habari Kanali Ali al-Sheikhi likisema.
Alisema mtu mmoja aliuawa, lakini shirika la habari la Reuters linamnukuu
rasmi akisema kuwa mtu mmoja aliyekuwa ndani ya helkopta alijeruhiwa wakati
helikopta alipopigwa kombora la kutungulia ndege.
CHANZO:http://bbc.co.uk/swahili
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top