Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Morsi akaidi amri ya jeshi

Rais Mohammed Morsi wa Misri

Katika hatua ya kulikaidi jeshi lenye nguvu nchini Misri, rais mpya Mohammed Morsi, ametoa amri kuwa bunge likutane.

Amri yake inakwenda kinyume na hukumu iliyotolewa mwezi uliopita na mahakama ya katiba, kwamba bunge la sasa siyo halali.

Bunge hilo lina wajumbe wengi wa vyama vya Kiislamu.

Hukumu ya mahakama ilitekelezwa na jeshi, ambalo lilifuta bunge na kujipa madaraka ya kutunga sheria.

Televisheni ya taifa inasema halmashauri ya jeshi itafanya kikao cha dharura kujadili amri ya Rais Morsi.

Chanzo:BBC Swahili

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top