Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA MAJI


              TAARIFA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA MAJI

                         TAARIFA KWA UMMA

Tarehe 9 Agosti 2012 Gazeti la Rai Na.995 katika ukurasa wake wa kwanza lilichapisha taarifa yenye kichwa cha habari “Ufisadi Wizara ya Maji” na kuwa Viongozi Waandamizi wanatumia mali za Serikali na taaluma zao kwa maslahi binafsi. Gazeti hilo lilieleza kuwa walinzi wanashirikiana na wafanyakazi kula “dili” za nje, habari hizi hazina ukweli wowote na ni za kupotosha umma.

Maelezo yaliyoandikwa katika uk.2 na 3 chini ya kichwa cha habari hiyo, hakuna uhusiano wa Wizara ya Maji na ufisadi katika hifadhi ya eneo la Ngorongoro ambayo inamhusisha Mh. Pius Msekwa, Makamu Mwenyekiti wa CCM kama Mwenyekiti wa Bodi hiyo. Kwa maoni yetu Gazeti la Rai linawajibika kukiri kuwa kichwa cha Habari hiyo kilikosewa tena ukurasa wa mbele (front page) kama ilivyoandikwa habari hiyo. Tunaheshimu Uhuru wa vyombo vya Habari na tungependa kama kuna suala lolote linalohitaji ufafanuzi, Wizara ipo tayari muda wowote kutoa maelezo badala ya kukimbilia kuandika habari zinazojichanganya.

Imetolewa na:Katibu Mkuu WIZARA YA MAJI   10/8/2012
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top