Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MBUNGE WA KIGAMBONI,MH.DK.FAUSTINE NDUNGULILE:SIPINGI UJENZI WA MJI MPYA KIGAMBONI


Mheshimiwa Faustine Ndugulile na Fina Mango baada ya kipindi cha Makutano, Magic FM
Mheshimiwa Ndugulile akisikiliza swali toka kwa Muendeshaji wa kipindi cha Makutano Fina Mango
Mbunge wa Kigamboni akijibu moja ya maswali aliyoulizwa  na wasikilizaji wa Kipindi cha Makutano.
 
Picha na Makutano Show-
-
Mbunge wa Kigamboni, Mheshimiwa Faustine Ndungulile amesema kamwe hajawahi kupinga ujenzi wa mji wa Kigamboni bali alitaka serikali imhakikishie kuwa wananchi wanashirikishwa katika hatua ya maamuzi  juu ya mradi wao. Mheshimiwa Ndugulile ameyasema hayo wakati akijibu swali kuhusu msimamo wake juu ya mradi huo katika kipindi cha Makutano, Magic FM. 

  Mradi huo ambao sasa ni miaka minne tangu uanze kuongelewa umezua mjadala mkubwa kwa wakazi wa Kigamboni, huku Mhe Ndugulile akitolewa kwenye moja ya vikao vya bunge la Jamhuri ya Muungano kutokana na msimamo wake juu ya mradi huo. 
 
Alisema tatizo la serikali imekuwa haitaki kufuata sheria  inayotaka ushirikishwaji wa wananchi kila hatua katika sera ya mipango miji. Pia aliongezea kusema wananchi wanataka majibu kuhusu lini mradi utaanza, wapi utaanzia, nini hatma yao hasa kuhusu fidia. 
 
Alipoulizwa swali na mmoja wa wanakigamboni kuhusu mgogoro  uliojitokeza baina yake na madiwani wa jimbo lake uliosababishwa na wao kutembelea moja vikao vya bunge kwa mualiko wa waziri wa ardhi na makazi Mhe Anna Tibaijuka, Ndugulile alijibu kuwa kwa sasa umeisha na kila mmoja ameshajua kosa lake.
 
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top