Kikosi cha Azam FC kipo katika hatua za mwisho za maandalizi kwa ajili ya kutetea Kombe la Mapinduzi 2013 litakaloanza jumatano ijayo visiwani Zanzibar.
Azam FC itaondoka baada ya Mwaka Mpya 2013 tayari kulitetea kombe hilo walilochukua mwaka huu katika fainali baada ya kuifunga 2-1 timu ya Jamhuri ya kutoka Pemba.
Kocha Msaidizi wa Azam FC, Kali Ongala ameiambia www.azamfc.co.tzkuwa wanajiandaa vizuri kuhakikisha wanarudi na kombe hilo kwa mara ya pili.
Kali amesema katika mashindano hayo watafanya kazi zaidi ya ilivyokuwa nchini Congo walipokuwa wanashiriki Kombe la Hisani kwa kuwa kikosi hicho kinawachezaji mahiri na wanaojua majukumu yao.
“Tumejiandaa na tuko vizuri, timu ina wachezaji wazuri wanaoweza kushindana hivyo sidhani kama tunaweza kulikosa kombe hilo, tunataka tulilete tena klabuni kwetu” amesema Kali.
Amesema kutetea ubingwa huwa ni kazi na kunahitaji maandalizi makubwa, kuzingatia hilo, wamewaandaa wachezaji katika hali zote, kuhakikisha hawapotezi nafasi hiyo muhimu kwao.
Ratiba kamili ya Mapinduzi Cup ni
2013 MAPINDUZI CUP [Zanzibar]:
AMAAN STADIUM
(January 2-12):
Group ‘A’:
Simba[Tanzania Mainland]
Tusker[Kenya]
Jamhuri[Zanzibar/Pemba]
Bandari[Zanzibar]
Group ‘B’:
Azam[Tanzania Mainland]
Mtibwa Sugar[Tanzania Mainland]
Coastal Union[Tanzania Mainland]
Miembeni[Zanzibar]
FIXTURES:
Wednesday, January 2:
4.00pm:Tusker v Bandari
8.00pm:Jamhuri v Simba
Thursday, Jan 3:
4.00pm:Mtibwa Sugar v Miembeni
8.00pm:Azam v Coastal Union
Friday, Jan 4:
4.00pm:Jamhuri v Bandari
8.00pm:Simba v Tusker
Saturday, Jan 5:
4.00pm:Mtibwa Sugar v Coastal Union
8.00pm:Miembeni v Azam
Sunday, Jan 6:
4.00pm:Tusker v Jamhuri
8.00pm:Simba v Bandari
Monday, Jan 7:
4.00pm:Miembeni v Coastal Union
8.00pm:Azam v Mtibwa Sugar
Tue, Jan 8:
REST DAY
Wed, Jan 9:
8.00pm:SEMI-FINAL I
Thur, Jan 10:
8.00pm:SEMI-FINAL II
Fri, Jan 11:
REST DAY
Sat, Jan 12:
8.00pm:FINAL
CHANZO:Azam Fc
Post a Comment