Wananchi wakiwa kwenye foleni ya kununua ving'amuzi vya Startimes eneo
la Bamaga jijini Dar es Salaam jana katika siku za mwisho kabla Mamlaka
ya Mawasiliano nchini (Tcra) kuhamisha matangazo ya televisheni kutoka
mfumo wa Analojia kwenda digitali.Picha na Silvan Kiwale
...........
Kwa ufupi
Hata hivyo, utata bado unagubika urushaji huo wa
chaneli za bure ambazo ni ITV, Star TV, TBC1, Channel Ten na Eat Africa
TV ikielezwa kuwa wamiliki wa vituo hivyo hawataki zionyeshwe bure
kwenye kila king’amuzi bali ving’amuzi vyao pekee.
...........
...........
Habari za ndani kutoka Mamlaka ya Mawasiliano
Tanzania (TCRA), zilizolifikia Mwananchi Jumapili, zinaeleza kuwa Jiji
la Dar es Salaam pekee, ndiyo litakuwa la kwanza kuingia kwenye mfumo
huo kuanzia Januari mosi, 2013 na siyo mikoa mingine nchini.
TCRA, imeshatangaza kuwa itaufunga mfumo wa analojia ifikapo Desemba 31 mwaka huu yaani kesho.
TCRA, imeshatangaza kuwa itaufunga mfumo wa analojia ifikapo Desemba 31 mwaka huu yaani kesho.
Habari hizo zimeeleza kuwa mamlaka hiyo imeamua
kuchukua hatua za tahadhari katika utekelezaji wa mpango huo muhimu, kwa
kuanza na mji mmoja baada ya mwingine, ambapo mwezi mmoja baada ya Dar
es Salaam kuanza kutumia mfumo wa dijitali, utafuatia Mkoa wa Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma
alipoulizwa aliliambia gazeti hili jana kwamba mamlaka yake itatoa
ufafanuzi kuhusu suala hilo leo katika mkutano wake na waandishi wa
habari.
“Hatuwezi kukurupuka katika suala hili, tuko
makini, lakini kesho (leo), tutakuwa na mkutano wa wanahabari kwa ajili
ya kueleza mikakati mbalimbali na jinsi tulivyojipanga katika jambo
hili,” alisema Profesa Nkoma.
Tayari TCRA imetaja miji mingine mbali ya Dar es
Salaam ambayo imeshaunganishwa katika mfumo wa dijitali kuwa ni pamoja
na Arusha, Mwanza, Tanga, Mbeya, Moshi na kwa sasa mji wa Morogoro
unajengewa miundombinu husika.
Habari zaidi zilieleza kuwa kwa utaratibu uliopo
sasa itachukua miezi kadhaa kabla ya kuzimwa kwa mfumo wa analojia
katika miji minane ya awali, ambapo pia itachukua muda mrefu zaidi
kuzimwa mfumo huo nchi nzima.
Shirika la Kimataifa la Mawasiliano (ITU),
limezitaka nchi zote duniani kuhamia kwenye mfumo huo wa kurusha
matangazo ya televisheni wa dijitali kutoka mfumo wa analojia ifikapo
Julai 2015.
Ikiwa nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika ya
Mashariki (EAC), Tanzania imeanza kutekeleza azimio la nchi hizo
ilizozitaka kufanya hivyo mwaka huu wa 2012, badala ya kusubiri hadi
tarehe ya mwisho iliyowekwa na ITU.
Wakati Tanzania ikiwa mstari wa mbele kuhamia
kwenye mfumo huo wa dijitali, ingawa kwa mtindo wa awamu, nchi nyingine
wanachama wa EAC hasa Kenya na Uganda bado hazijaingia katika mfumo huo.
TCRA imezikabidhi kampuni tatu kufanya kazi ya
usambazaji wa mfumo huo wa dijitali, ambazo ni Basic Transmissions
inayoundwa na Kampuni za IPP Media na Sahara
Communications, Kampuni ya Ting ya Agape Associates na Star Media Tanzania Limited (Startimes) ambayo ina ubia na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Star Communications and Technology ya China.
Communications, Kampuni ya Ting ya Agape Associates na Star Media Tanzania Limited (Startimes) ambayo ina ubia na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Star Communications and Technology ya China.
TCRA imekuwa ikielezea kuwa Tanzania ipo tayari
kujiunga na mfumo huo kwa kuwa asilimia kati ya 22 kati ya 24 ya nchi
ambayo inatumia analojia, tayari imefikiwa na mtandao wa mfumo wa
dijitali, ikijumuisha miji minane ambayo kwa kiasi kikubwa kampuni ya
Startimes imeifikia.
Hata hivyo, baadhi ya watu wameshindwa kuzielewa takwimu hizo
kwa kuwa mitambo ya analojia ipo katika mikoa kadhaa nchini, ambayo bado
haijapata mfumo wa dijitali. Mikoa hiyo ni pamoja na Lindi, Tabora,
Bukoba, Musoma, Kigoma na Singida.
Kampuni ya Startimes ndiyo inayoongoza kwa kuwa na
wateja wengi ambapo hadi sasa inakadiriwa kufikisha wateja 350,000,
Kampuni ya Ting ikiwa na wateja 10,000, huku Kampuni ya Basic
Transmissions ikitangaza kuanza shughuli zake hivi karibuni.
Bei ya king’amuzi ni Sh39,000 ingawa mnunuzi anapaswa kulipia fedha za ziada kwa ajili ya kifurushi atakachochagua.
Bei ya king’amuzi ni Sh39,000 ingawa mnunuzi anapaswa kulipia fedha za ziada kwa ajili ya kifurushi atakachochagua.
Hata hivyo, utata bado unagubika urushaji huo wa
chaneli za bure ambazo ni ITV, Star TV, TBC1, Channel Ten na Eat Africa
TV ikielezwa kuwa wamiliki wa vituo hivyo hawataki zionyeshwe bure
kwenye kila king’amuzi bali ving’amuzi vyao pekee.
TCRA imeeleza kuwa kwa sasa imefanikiwa kupata ufumbuzi wa muda, ambapo chaneli zote zinaweza kuonekana bure kwenye kila king’amuzi.
TCRA imeeleza kuwa kwa sasa imefanikiwa kupata ufumbuzi wa muda, ambapo chaneli zote zinaweza kuonekana bure kwenye kila king’amuzi.
Wananchi wachangamkia ving’amuzi
Katika hatua nyingine, gazeti hili lilifika katika ofisi za makao makuu ya Startimes jijini Dar es Salaam na kukuta mamia ya wananchi wakiwa katika foleni ya kununua ving’amuzi hivyo.
Katika hatua nyingine, gazeti hili lilifika katika ofisi za makao makuu ya Startimes jijini Dar es Salaam na kukuta mamia ya wananchi wakiwa katika foleni ya kununua ving’amuzi hivyo.
Baadhi ya wananchi hao walionyesha masikitiko yao
baada ya kufutwa kwa malipo ya mwezi ya Sh9,000, badala yake kubaki
malipo ya Sh23,000 na 36,000 kwa mwezi.“Kwa sasa wametoa ofa, ukinunua
king’amuzi kwa Sh39,000 utalipia malipo ya mwezi ya kati ya Sh13,000 au
Sh23,000, kile kifurushi cha bei nafuu wamekifuta na hivyo kusababisha
usumbufu mkubwa,” alisema Hadji Jumanne mkazi wa Kijitonyama.
Naye Happy Lazaro alisema Serikali inatakiwa
kuongeza muda ili kuwapa fursa wananchi kununua ving’amuzi hivyo kwa
kuwa hivi sasa imekuwa vurugu na huenda mitambo ya analojia ikazimwa
huku wengi wakiwa hawajapata ving’amuzi hivyo.
Hata hivyo, watendaji wa kampuni hiyo waligoma
kuzungumzia changamoto mbalimbali zinazotolewa na wateja wao ikiwa ni
pamoja na ubovu wa baadhi ya ving’amuzi, mabadiliko ya bei ya vufurushi
kwa maelezo kuwa siyo wasemaji.
CHANZO:MWANANCHI
CHANZO:MWANANCHI
Post a Comment