Ofisi za
Kampuni ya Renex iliyopo Lisbon,RENEX ni Kampuni ya mabasi nchini
Ureno.Eneo la Kampuni hiyo linaonekana likiwa safi muda wote likiwa na
vifaa vya kutupia taka na vyoo safi kwa wasafiri watumiao Mabasi
hayo.Hali ni tofauti ukija hapa Nyumbani ambapo tumeshuhudia uchafu na
kutojali afya za wasafiri hivyo mtu anapoamua kusafiri hupata shida
kuanzia anapofika eneo la kupandia basi kutokana na mpangilio mbovu wa
huduma mbalimbali kwa wasafiri.Haya tumekuwa tukiyashuhudia Kituo kikuu
cha Mabasi yaendayo mikoani ikiwa ni pamoja na kulanguliwa tiketi.
Zawadi toka Lisbon, Ureno kuelekea Sikukuu za Christimas na Mwaka mpya kwa wale wasafiri.Suala la Usalama ni muhimu sana kwa wewe msafiri na ungependa usafiri kwa usafiri wa uhakika na salama.NImepiga picha hii ili kuwakumbusha ndugu jamaa na marafiki kuwa wanaposafiri hususani kipindi hiki cha Disemba suala la usalama ni muhimu sana hasa basi watakalopanda ili waweze fika salama.
Kipindi hiki huwa tunashuhudia baadhi ya wafanyabiashara ambao hawajali usalama wa abiria wakitoa mabasi yao gereji ili mradi tu avune pesa na kuwasumbua abiria kwa gari kuharibika mara kwa mara liwapo barabarani.
PICHA NA MDAU WETU
Post a Comment