Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CCM ARUSHA YACHACHAMAA UCHAGUZI NEC LONGIDO


Kwa ufupi
Habari za uhakika toka ndani ya wajumbe wa kikao hicho, zimeeleza kuwa kikao hicho, ambacho kiliongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo Ole Nangole, kilifikia uamuzi wa kurejewa uchaguzi huo, baada ya kuridhika kuwa Laizer hakupata nusu ya kura katika uchaguzi huo.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
KAMATI ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Arusha, imependekeza kurejewa uchaguzi wa nafasi ya mjumbe wa Halmashauri Kuu(Nec) kutoka Wilaya ya Longido nafasi ambayo awali Mbunge wa jimbo hilo, Lekule Laizer alitangazwa kushinda.
Habari za uhakika toka ndani ya wajumbe wa kikao hicho, zimeeleza kuwa kikao hicho, ambacho kiliongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo Ole Nangole, kilifikia uamuzi wa kurejewa uchaguzi huo, baada ya kuridhika kuwa Laizer hakupata nusu ya kura katika uchaguzi huo.
Mjumbe mmoja wa kamati hiyo, alisema katika uchaguzi huo wa Nec mwaka mwa jana, uliofanyika mwishoni mwaka jana,na kusimamiwa na Katibu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Arusha, George Kijazi Laizer alipata kura 417,Peter Lemshau kura 381 na Michael Sakino kura 58.
“Katika uchaguzi huo, kura halali zilikuwa ni 871 na kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, hapa hakupatikana mshindi na Laizer na Lemshau wanapaswa kurudia uchaguzi lakini cha ajabu Laizer alitangazwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda kuwa ni mjumbe wa NEC”alisema mjumbe huyo.
Mjumbe huyo alisema mapendekezo hayo, tayari yamepelekwa sekretarieti ya CCM taifa na yanatarajiwa kutolewa uamuzi na kamati kuu ambayo inatarajiwa kupatikana mwishoni mwa wiki hii.
Hata hivyo, wakati kamati ya siasa mkoa ikipendekeza kurejewa kwa uchaguzi huo, tayari kuna uvumi kuwa, Laizer huenda akateuliwa kugombea nafasi ya kamati kuu ya CCM hasa kutokana na kuungwa mkono na vigogo kadhaa wa chama hicho.
“Tumepata taarifa kuwa atateuliwa kugombea kamati kuu,sasa hili litakuwa ni jambo la ajabu kwani bado hajawa mjumbe wa NEC kwa nini ateuliwe kuwa mjumbe wa kamati kuu”alihoji kiongozi huyo.
Kwa upande wake, Lemshau alipotakiwa kuelezea hatma yake alisema anasubiri maamuzi ya ngazi za juu kwani tayari alipeleka vielelezo vyake.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Arusha, Issack Joseph alipotakiwa kuelezea maamuzi ya kamati ya Siasa ya mkoa kuhusiana na kurejewa kwa uchaguzi huo wa NEC Longido ,alisema kikao cha kamati kuu ni cha siri,hivyo lakini hata hivyo hakukanusha wala kukubali kama walipendekeza kurejewa uchaguzi huo.

NA MWANANCHI

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top