Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

ANSAF YASHAURI SIFA ZA DIWANI


Ansaf Tanzania.
Jukwaa Huru la Kilimo nchini (Ansaf), limeshauri kuwapo kwa kigezo cha walau kufaulu elimu ya kidato cha nne kama moja ya sifa za kuwa diwani.
Ushauri huo uko kwenye ripoti ya jukwa hilo  iliyotolewa juzi jijini Dar es Salaam kufuatia utafiti lililoendesha kwa miaka mitatu iliyopita katika wilaya sita nchini.
Utafiti huo ulifanyika katika wilaya za Karagwe, Tandahimba, Singida, Ulanga, Korogwe na Iringa.
 
Ripoti hiyo ‘Ufuatiliaji wa Uwajibikaji wa kijamii wa Sekta ya Kilimo,’ inaainisha pamoja na mambo mengine, namna serikali za mitaa katika ngazi za wilaya zinavyotenga kiasi kidogo cha bajeti kwenye sekta ya kilimo, bila kuzingatia mchango wake kwenye uchumi.
 
Akizungumza wakati wa kutoa ripoti hiyo kwa wadau mbalimbali wakiwamo waliotoka nje ya nchi, Mkurugenzi Mtendaji wa Ansaf, Audax Rukonge, alisema kitendo hicho kinatokea kutokana na madiwani wengi kuwa na elimu ya darasa la saba.
 
“Moja ya mambo yaliyogunduliwa na utafiti ni kilimo kutengewa fedha kidogo ingawaje ndicho kinachotoa kati ya asilimia 20 hadi 60 ya mapato ya vyanzo vya ndani ya wilaya, huku madiwani wakishindwa kuhoji,” alisema.
 
Rukonge alisema pamoja na bajeti ndogo kutengwa kwenye sekta ya kilimo na watendaji, ripoti hiyo imegundua pia kuwapo kwa matumizi mabaya ya fedha za umma, huku madiwani ambao ni moja ya vyombo vya udhibiti katika ngazi ya wilaya wakishindwa kuhoji.
 
Rukonge alisema wawakilishi hao wanashindwa kuhoji pale fedha zinapohamishwa kwenda kwenye miradi isiyokusudiwa kutokana na kutokuwa na ufahamu wa lugha zinazotumika kwenye bajeti kwa wengi wao wana elimu ya msingi isiyowapa maarifa ya kuielewa lugha ya kifedha.
 
“Lakini wakati mwingine wanakosa taarifa za kutosha toka kwa watendaji ili kuwawezesha kufuatilia matumizi, na kwa kuwa hawana elimu stahili wanashindwa kuhoji, wakati suala la wao kupatiwa taarifa za matumizi ni haki yao,” alisema.
 
Rukonge alisema kutokana na udhaifu huo, watendaji wa halmashauri hutoa nyaraka za taarifa mbalimbali siku moja au mbili kabla ya kikao cha madiwani, muda ambao hauwapi madiwani fursa ya kuzisoma na kuwa na maswali ya kuhoji.
 
CHANZO: NIPASHE
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top