Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

SERIKALI:MABADILIKO DIGITALI HAYAEPUKIKI

SERIKALI imesema mabadiliko ya utangazaji kutoka analojia kwenda dijitali hayaepukiki.
Kutokana na hali hiyo imewataka wadau wote kushirikiana katika mchakato mzima kama ilivyokubalika kupitia vikao mbalimbali vilivyofanyika tangu mwaka 2005.
Akitoa tamko la serikali kuhusiana na uhamaji huo jana, Waziri wa Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa alisema serikali imejiridhisha kuwa mchakato wote wa kuelekea mfumo huo wa utangazaji ulifanywa kwa umakini mkubwa na kwa muda wa kutosha na kuwa elimu imetolewa na inaendelea kutolewa.
“Ni dhahiri kuwa watoa huduma za miundombinu ya dijitali waliopewa leseni tangu 2010 wameendelea na wajibu wa kuweka mitambo ya digitali sehemu mbalimbali nchini na zoezi linaendelea vizuri,” alisema Profesa Mbarawa.
Alisema serikali haitavumilia kikundi au mtu yeyote atakayeonekana kupotosha au kufifisha mchakato wa kuhamia katika mfumo wa utangazaji wa dijitali.
Aidha, alisema serikali imeiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuendelea na utaratibu, ratiba ya uzimaji wa mitambo ya analojia kama ilivyotolewa na serikali.
Pia serikali imeiagiza mamlaka hiyo kupitia kamati ya maudhui kuchunguza endapo kauli zilizotolewa na baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari kwa kutumia muda mrefu kuelezea kauli zao katika vyombo vyao vya habari kama hawakukiuka sheria na kanuni za Utangazaji kwa nia ya kupotosha umma kwa kusudio la kudhoofisha maamuzi hayo ya serikali.
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwapo na kauli mbalimbali zinazotolewa na baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari na hasa wa utangazaji wakiilaumu na kuishutumu serikali kuhusu uamuzi wa kuhamia katika mfumo wa dijitali.
Waziri Mbarawa alisema kauli hizi sio za kweli, zinapotosha ukweli na hali halisi na pia zinalenga kuchochea wananchi kutokubaliana na uamuzi wa serikali.
Waziri Mbarawa aliwaomba wananchi kupuuza upotoshaji unaofanywa kuhusu ukweli wa mabadiliko ya mfumo wa utangazaji wa kutoka analojia kwenda dijitali. 

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top