Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TASWIRA:MKURUGENZI WA ASIA NA AUSTRALASIA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akiongea na Mhe. Lv Youqing, Balozi wa China hapa nchini masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na China ikiwa ni pamoja na matarajio ya nchi hizi mbili baada ya ziara ya Rais wa China, Xi Jinping aliyoifanya hapa nchini mwezi Machi, 2013.


Balozi wa China hapa nchini Lv Youqing akifafanua jambo kwa Balozi Kairuki wakati wa mazungumzo yao.

Balozi Kairuki na Balozi Lv Youqing wakiendelea na mazungumzo huku wajumbe waliofuatana nao wakisikiliza. Kulia ni Bw. Medard Ngaiza, Afisa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Asia na Australasia. Wengine ni Bi. Fang Wang, Afisa katika Ubalozi wa China na Bw. Lin Zhiyong (kushoto kwa Bi. Fang), Afisa Mkuu wa Ofisi ya Biashara na Uchumi ya Serikali ya China hapa nchini.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top