Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

UVCCM KILIMANJARO WAPINGA MAANDAMANO

 
    
Moshi. Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoani Kilimanjaro umesema hautafanya maandamano yoyote yasiyo na tija na badala yake wataweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili ikiwamo ya ukosefu wa ajira.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kilimanjaro, Frederick Mushi alitoa ahadi hiyo juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Mawazo mjini Moshi baada ya kuzindua tawi jipya la vijana wa eneo hilo.
Mushi alielezea kusikitishwa kwake na baadhi ya wanasiasa wanaowatumia vijana kufanya maandamano ili kutimiza malengo yao ya kisiasa huku vijana wakipata shida.
Alisema vijana hao wa mawazo ni mfano wa kuigwa na uamuzi wao utawafungulia milango ya kujiletea maendeleo hapo baadaye.
Kwa upande wake, Kamanda wa Vijana UVCCM Wilaya ya Moshi mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kupitia Moshi mjini, Aggrey Marealle alishauri vijana hao kuanzisha Chama cha Kuweka na Kukopa (Saccos).
Shambe Sagaf, ambaye alimwakilisha Marealle alisema kuwa njia ya pekee ya vijana kupambana na tatizo la ajira ni kujiunga na kuanzisha vikundi vya maendeleo ambapo aliahidi kuwaunga mkono ili waweze kutimiza azma yao.
Mwenyekiti wa UVCCM Moshi Mjini, Abdalla Thabit alisema mapema kikundi hicho kilianzishwa na vijana hao kikiwa na lengo la kujitegemea kwa kuanzisha miradi mbalimbali.    

NA MWANANCHI
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top