Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CHADEMA YASUSIA GHAFLA KONGAMANO

Mkurugenzi wa Oganaizesheni na mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila (Kushoto) akizungumza kuhusu chama hicho kugomea kungamano la Amani, lililoandaliwa  na kijtuo cha demokrasia Tanzania (TCD) Mwingine ni mratibu wa kanda ya Ziwa Mashariki Renatus Nzemo.Picha na Michael Matemange  

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana kilitangaza kwamba hakitashiriki kongamano la amani linalotarajiwa kufanyika kwa siku mbili kuanzia leo baada ya kuitishwa na  Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) jijini Dar es Salaam.
Kongamano hilo linatarajiwa kujadili na kutafakari  amani ya taifa, lakini chama hicho kimesema hakitahudhuria kwa sababu kongamano lina mkono wa Serikali.
Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo wa Chadema, Benson Kigaila, alisema amani haijadiliwi kwenye kufanya makongamano ya hotelini bali mazingira ya amani yanawekwa na Serikali kwa kutenda haki.
Akifafanua jana, Kigaila alisema  Chadema inaamini kwamba Serikali ni mfadhili wa kongamano hilo na kwamba  haitashiriki kwa kuwa amani haijadiliwi bali inatengenezwa na kuwapo kwa mazingira ya haki na usawa.
 ‘’Chadema haitashiriki mkutano huo kwa kuwa aliyepanga, aliyefadhili na aliyeitisha mkutano huo kwa mgongo wa TCD, ni Waziri Mkuu, Mizengo  Pinda, ambaye ndani ya nafasi yake, haonekani kuwa na dhamira ya dhati ya kuwapo amani katika taifa letu,’’ alisisitiza.
Pia alisema  Chadema haitashiriki katika mkutano huo akisema Serikali ya CCM, imejaa unafiki kwa kuhubiri amani mchana, wakati usiku inachochea uhasama wa kidini, kisiasa na inawagawa Watanzania kwa misingi ya imani za kidini na vyama.
 Mwenyekiti wa TCD, James Mbatia alipoulizwa juu ya madai ya Chadema kwa njia ya simu jana jioni alisikitishwa na madai hayo akisema kongamano hilo limeitishwa kutekeleza uamuzi wa kikao cha vyama vya upinzani kilichofanyika Februari 9, mjini Dodoma baada ya kufukuzwa ndani ya Bunge,  John Mnyika ambaye ni Mbunge wa Ubungo kupitia Chadema.Alisema gharama za kongamano hilo hazizidi Sh100 milioni na kwamba  fedha hizo zinatoka kwa wafadhili wa TCD na Serikali imechangia kidogo.Mbatia alisisitiza kwamba wakiwa Dodoma kipindi hicho walikubaliana kuitisha makongamano ya aina hiyo yakiwashirikisha wadau mbalimbali kwa awamu tofauti na kwamba kwa sasa vimealikwa vyama vyenye wabunge  bungeni na Chama cha UPDP ambacho kitawakilisha vyama ambavyo havina wabunge.  ‘’Sasa ni mwanzo, makongamano mengine yataitishwa yakiwashirikisha wadau mbalimbali,’’ alisema.
Alisema Waziri Mkuu Pinda hahusiki  kwenye kongamano hilo, bali Serikali itawakilishwa na  wawakilishi 20 wakiwamo wa kutoka Zanzibar. Mbatia ambaye ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi  aliwashangaa Chadema kwa kugeuka ghafla akisema hata ratiba walishiriki.

CHANZO:MWANANCHI
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top