Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KUTOKA GAZETI LA MWANASPOTI:MESSI WA SIMBA SASA CHINI YA ULINZI MKALI



 Pluijm  raia wa Uholanzi,  alitua katika mchezo huo akiwa na peni na karatasi akiwa na kiongozi mmoja wa Yanga, Hafidh Saleh, alisema jambo lingine lililomshangaza katika kikosi cha Simba ni uwezo wa Messi na Kiemba ambao kwake wanahitaji kuchungwa sana.  
,,,,,,,,,,,,,,,,
MZUNGU wa Simba, Zdravko Logarusic aliibuka kimyakimya Jumamosi kuangalia Yanga ikicheza na Ashanti, akasoma ufundi wa kocha mpya wa Jangwani, Hans Pluijm na kuishia zake.
Logarusic aligoma kutamka chochote alichokigundua kwenye staili ya soka la Yanga mpya ya Pluijm ambaye ni kama mtani wake kwa vile wanajua vilivyo ndani na nje ya uwanja.
Lakini siku inayofuata Pluijm naye akaibuka Taifa kuiangalia Simba ambayo hakuwahi kuiona tangu asaini Yanga. Unajua alichosema?  “Mbona wanacheza nyuma ya mpira tu?” Lakini mechi ilipomalizika akaondoka na jina la Ramadhan Singano ‘Messi’ na Amri Kiemba kwenye kitabu chake.
Akizungumza na Mwanaspoti wakati akiishuhudia Simba ikiiangamiza Rhino ya Tabora kwa bao 1-0, juzi Jumapili katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Pluijm alisema ameuangalia mchezo huo, lakini amebaini kwamba Simba inajilinda zaidi kama ilivyokuwa kwa Rhino kitu ambacho hakikumvutia hata kidogo.
Pluijm  raia wa Uholanzi,  alitua katika mchezo huo akiwa na peni na karatasi akiwa na kiongozi mmoja wa Yanga, Hafidh Saleh, alisema jambo lingine lililomshangaza katika kikosi cha Simba ni uwezo wa Messi na Kiemba ambao kwake wanahitaji kuchungwa sana.
Alisema kwa upande wa Messi ni nyota muhimu Simba ambaye ni msumbufu kwa mabeki na ana uwezo wa kuzuia wachezaji wa timu pinzani wasipande kusababisha madhara kwa Simba huku Kiemba akimuelezea kwamba anajiamini na anatoa pasi za uhakika.
“Sikuona soka ya kuvutia sana, ilipooza hakukuwa na mpira wa presha, Simba inacheza taratibu na inajilinda sana ndiyo maana mpira haunogi,”alisisitiza kocha huyo na kudai kwa ukubwa wa Simba ilipaswa kushambulia si kujilinda.
“Nimefurahishwa sana na uwezo wa yule mwenye namba 11(Messi) mgongoni ni hatari sana anastahili ulinzi muda wote, hata yule namba 28 (Kiemba) yuko vizuri sana,”alisema.
Kocha huyo wa Yanga alikuwa hajaiona Simba awali kwani aliposaini mkataba na Yanga alikwenda moja kwa moja kambini Uturuki hadi aliporejea wiki iliyopita. Makocha hao wanajuana vilivyo kwani wamewahi kufanya kazi kwenye timu tofauti katika Ligi ya Ghana.
Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic alikuwa uwanjani kuiangalia Yanga ikicheza na Ashanti United lakini hakutamka lolote kuhusiana na mabadiliko aliyoyaona kwa kocha mpya wa Jangwani.

CHANZO:Mwanaspoti
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top