Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

'AG Z'BAR':IPO SIKU UKWELI UTADHIHIRIKA


Dar es Salaam. Kung’olewa kwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman katika nafasi hiyo ni kama kumewasha moto visiwani humo huku mwenyewe akisema: ‘Ipo siku ukweli utadhihirika.’
Othman licha ya kutafutwa kutwa nzima ya jana, hakuwa tayari kuzungumzia kufukuzwa kwake kazi na badala yake alituma ujumbe mfupi kupitia simu yake ya kiganjani akisema: “Si wakati wake kulizungumza.”
Alipoulizwa kwamba pengine anaweza kuwa tayari lini kuzungumzia suala hilo, Mwanasheria huyo aliyepinga baadhi ya Ibara za Katiba zinazopendekezwa kwa kuzipigia kura za hapana, alijibu pia kwa kifupi: “I have no idea when (sifahamu ni lini), time will tell (ipo siku ukweli utadhihiri)”.
Kwa upande mwingine, watu wa kada mbalimbali nchini wameelezea uamuzi wa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kumtimua kazi kuwa ni uonevu kwa kuwa alitumia haki yake ya kikatiba.
Mwalimu wa Idara ya Lugha za Kigeni na Isimu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Faraja Christoms alisema, “Sidhani kama ni matumizi mazuri ya madaraka. Othman katika maelezo yake alitamka wazi kuwa maoni yake si msimamo wa Serikali ya Zanzibar. Alichokizungumza ndiyo msimamo wake binafsi na jinsi anavyoona inafaa.”
Alisema Mwanasheria huyo katika maoni yake alieleza wazi jinsi Katiba ya Zanzibar inavyokinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano... “Kilichomtokea ni tatizo la kutokuwapo kwa maridhiano tangu ulipoanza mchakato wa kuandika Katiba Mpya.”
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na masuala ya kijamii (Fordia), Buberwa Kaiza alisema wajumbe wa Bunge la Katiba walipiga kura kwa utashi wao na si ushawishi kutoka katika makundi wanayotoka.
“Alichokizungumza Othman si maoni ya Serikali za Zanzibar. Alipokuwa bungeni alikuwa sawa na wajumbe wengine na si mwakilishi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Hii ni ishara mbaya kwa watendaji wa Serikali. Maana yake ni kwamba watendaji wa chini wakifichua uovu unaofanywa na walio juu yao wanaweza kufukuzwa kazi.”
Mtaalamu wa Lugha ya Kiswahili, Dk Aldin Mutembei alisema: “Sasa watu wameanza kuzuiwa kuamua mambo yao wao wenyewe. Othman alipiga kura kama yeye binafsi na si Serikali ya Zanzibar tena akiwa na mawazo huru kabisa. Kumfukuza kazi ni kutomtendea haki.”
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema: “Ubatili siku zote huzaa ubatili. Nchi yetu sijui inakwenda wapi, maana watu wanazuiwa kufanya mambo yao ambayo yapo kikatiba. Maandamano hakuna, ukisema ukweli unafukuzwa kazi?
“Watanzania wataendelea kudai Katiba yenye maoni yao. Hii ni ishara ya kutaka kuwafumba midomo wengine wanaopenda kueleza ukweli.
Mhadhiri wa UDSM, Dk Benson Bana alikuwa tofauti na wenzake, akisema kilichomkuta mwanasheria huyo alikitarajia kwa sababu kitendo chake cha kupiga kura ya hapana kilimaanisha kuwa amekwenda tofauti na msimamo wa Serikali ya Zanzibar.

Habari zaidi Endelea Hapa>>>> 

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top