Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KAJALA ASHAMBULIWA MTANDAONI

Kupitia mtandao maarufu wa picha wa kijamii, mwanadada Kajala amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuweka picha ya simu aina ya samsung galaxy note 4 kwenye account yake kuwa anamiliki simu hiyo ilihali simu yenyewe ikiwa bado hata haijaanzwa kuuzwa sehemu yoyote duniani. Kupitia picha hiyo kajala aliambulia maneno kadhaa ya kashfa toka kwa watu mbalimbali wengi wao wakimtaka aache maisha ya kuigiza.




 
 
“Hahahaha watu ndo wanatoa pre order october 16 ndo ina launched we umeitoa wap wakat bado haijaanzwa kuuzwa!dah!kwel sasa naanza kumin maisha yako ni ya kuigiza nakufata mkumbo mumy…pole” 
 
“Duh … Simu aijatoka hiyo Pre Order imeanza USA & UK tarehe 19/09 lkn retail stores wanaanza kuuza tarehe 17/10 , hiyo pre order kwa watu ambao awataki kumiss ikitoka wanalipia kabisa ikitoka unaenda kuchukua , sasa hiyo umenunua wapi mwenzetu…” 
 
“KAJALA ACHA UONGO HII CM LABDA MCHINA ORIGINAL HAIJATOKA MPAKA KWA ORDER LOO MWANAMKE MZIMA MPKA LEO UNARINGISHIA CM PAULA NAE AFANYE NINI”
 
Wewe unaonaje kuhusu jambo hili la mastaa nchini kuishi maisha ya kuigiza kwa ajili ya kuonekana wapo juu kwa mashabiki wao?!
 
Kwa Hisani ya Matukio Tz.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top