Mgombea
urais wa CHADEMA kupitia UKAWA Mh Edward Lowassa leo anatarajia
kuzungumza na makundi mbalimbali ya wanawake kabla ya uzinduzi wa
kampeni kwa kueleza mipango alionayo katika kuinua uchumi wa wanawake
na kupambana na umasikini
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama hicho Mh.Halima Mdee akizungumza jijini Dar es Salaam jana amesema Mh Lowassa pamoja na viongozi mbalimbali wa CHADEMA, watazungumza na wawakilishi wa makundi mbalimbali ya wanawake ambapo atazungumza mikakati alionayo kwa wanawake na watoto na hatma ya maendeleo kwa taifa
Aidha Mdee amesema Lowassa atapata fursa ya kuainisha kuhusu watoto wa kike wanaokosa fursa za elimu , sekta ya kilimo ambayo ina ajiri wanawake wengi pamoja na sekta ya afya.
Katika hatua nyingine ya Kampeni Mdee amesema BAWACHA wamegawa kanda kumi kuhakikisha wanawafikia wanawake katika mikoa yote kupeleka ujumbe wa matumaini kwa wanawake kushiriki harakati za ukombozi kwa taifa lao
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama hicho Mh.Halima Mdee akizungumza jijini Dar es Salaam jana amesema Mh Lowassa pamoja na viongozi mbalimbali wa CHADEMA, watazungumza na wawakilishi wa makundi mbalimbali ya wanawake ambapo atazungumza mikakati alionayo kwa wanawake na watoto na hatma ya maendeleo kwa taifa
Aidha Mdee amesema Lowassa atapata fursa ya kuainisha kuhusu watoto wa kike wanaokosa fursa za elimu , sekta ya kilimo ambayo ina ajiri wanawake wengi pamoja na sekta ya afya.
Katika hatua nyingine ya Kampeni Mdee amesema BAWACHA wamegawa kanda kumi kuhakikisha wanawafikia wanawake katika mikoa yote kupeleka ujumbe wa matumaini kwa wanawake kushiriki harakati za ukombozi kwa taifa lao
Chanzo: East Africa Television (EATV)
Post a Comment