Siku ya Jumanne oct 27,2015 usiku vikosi vya serikali ya mapinduzi
zanzibar vilingia katika maeneo ya Muembe Tanga karibu na Makao Makuu ya
CUF Mtendeni na kufyetua risasi juu na kupiga watu kwa magongo huku
wakivunja madirisha na milango ya nyumba tatu katika eneo hilo la
Mwembetanga. Mwandishi wetu Salma Said alitembelea eneo hilo na
kuzungumza na Mama Bimkubwa Mussa, Mwalimu wa Madrasa mwenye umri wa
miaka 75 na kwanza ameeleza kilichotokea.Sikiliza matangazo yetu ya hivi
punde.
Huku muda ukiyoyoma kuelekea siku ya mwisho kabisa kisheria ya
kutangazwa kwa matokeo ya urais Zanzibar, vyama vidogo vidogo
vilivyoweka wagombea wa urais katika uchaguzi huo vinaishinikiza tume ya
uchaguzi Zanzibar ZEC kutoa matokeo haraka ili kuiyepusha nchi
kuendelea kuwa katika hali ya sintofahamu. Sikiliza matangazo yetu ya
leo mchana.
SOURCE:DW KISWAHILI
Post a Comment