Ligi kuu ya Tanzania bara iliendelea
kutimua vumbi katika viwanja Sita ambapo mabingwa watetezi ligi hiyo
Yanga ikiwa ugenini huko Shinyanga ilikwenda sare ya mabao 2-2 na Mwadui
Fc.
Wekundu wa msimbazi wakicheza katika uwanja wa Taifa Jijini
Dar es Salaam walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wagosi wa kaya
Coastal Union
Toto African ikawatambia timu ya Mgambao Shooting
kwa kuwachapa kwa bao 1-0, huku wakata miwa wa Mtibwa Sugar wakipata
ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wakata miwa wenzao wa Kagera Sugar.
Mbeya
City wakicheza katika uwanja wao wa Sokoine wakaenda sare ya 1-1 na
Majimaji, nao Ndanda wakiwa katika uwanja wao wa Nangwanda sijaona
walienda sare ya bila kufungana na Stand United
Post a Comment