Serikali ya Marekani imestushwa sana na tamko la hivi karibuni la
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ambapo ametamka kusudio lake
la kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais wa Zanzibar.
Hatua hii inasitisha mchakato wa uchaguzi uliofanyika vizuri na kwa
amani, kama ilivyo elezwa na waangalizi wa uchaguzi kutoka Ubalozi wa
Marekani, Jumuiya ya Ulaya, Jumuiya ya Madola na Jumuiya ya Maendeleo ya
Nchi za Kusini mwa Afrika pamoja na kusitisha zoezi la majumuisho ya
kura lililokuwa linakaribia kukamilika.
Tunatoa wito wa kuondolewa kwa tamko hilo na kuzisihi pande zote
kudhamira kwa dhati kuukamilisha mchakato huu wa kidemokrasia kwa uwazi
na kwa Amani. Watu wa Zanzibar wanastahili jambo hilo.
Chanzo: US Embassy Tanzania
Post a Comment