Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KAMATI KUU(CC) YA CCM YAMPONGEZA RAIS MAGUFULI


Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho kikwete akiongozana na Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli , Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Mhe Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015.


Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho kikwete akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015.


Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipigiwa saluti na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015.


Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim. wengine ni Waziri Mkuu Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mhe samia Suluhu Hassan na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahmana Kinana kabla ya kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es salaam leo Desemba 7, 2015. 

 Kamati Kuu ya CCM (CC) iliyoketi leo hii chini ya Mwenyekiti Jakaya Kikwete imempongeza Rais Magufuli kwa mapambano aliyoyaanzisha na kumtia moyo kuwa CCM,kwa ujumla wake,iko pamoja naye.
Lakini,CC imemshauri na kumtaka Rais Magufuli kujiridhisha vya kutosha kabla ya kutumbua majipu mbalimbali ya kitaifa. Imesemwa kuwa nchi yaweza kuendeshwa kwa majungu na hivyo wananchi kuishi kwa visasi na kuchongeana. Ni kama CC imemfunga Speed Governor Rais Magufuli 'kimtindo'.

Pia,CC imemtaka kuwa makini na teuzi zake za sasa na zijazo. Imedhihirika leo kuwa Rais Magufuli alikuwa akisubiri kikao cha CC ili kuteua na kutangaza Mawaziri. Sasa mambo yatafanyika!
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top