Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

JULIUS MTATIRO AHOJI UKIPEWA SHS.LAKI NNE UTAWEZA KUENDESHA SHULE MWEZI MZIMA ?

UKIPEWA SHS. LAKI NNE UTAWEZA KUENDESHA SHULE MWEZI MZIMA?
Mpango wa serikali wa elimu bure unaonesha kuwa serikali inatenga shilingi elfu kumi (10,000) kwa mwaka mzima kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi. Hiyo ina maana kwamba kila mwanafunzi anapelekewa shilingi 833 za kutumia mwezi mzima - kama shule ina wanafunzi 500 inapelekewa shilingi 416,500 kwa mwezi.


Kama shule moja ina walinzi wawili na inawalipa shs 150,000 kwa mwezi mmoja ina maana fedha zinazotumwa zinaishia kwa walinzi na kubakiza shilingi 116,500. Hizi zikitumika kulipa maji na umeme haibakii hata senti tano. Nimeongea na baadhi ya walimu wakuu wanasema wamechanganyikiwa na hawajui cha kufanya.


Sijui kama mahitaji ya shule zetu yamekamilika? Hebu serikali ijipange zaidi ili tusije kuzua bomu jingine kwenye elimu. “Pump more money on education”, hakuna njia nyingine!
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top