Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KITONGOJI CHA KITANEWA JIMBONI KWA LUKUVI HATARI KUTOWEKA, CHAZINGIRWA NA MAJI





KITONGOJI cha Kitanewa katika kijiji cha Mapogoro, tarafa ya Idodi wilayani Iringa mkoani Iringa, jimboni Isimani kwa Waziri wa Ardhi William Lukuvi kimeendelea kuathiriwa na mafuriko na kuwa katika hatari  ya kutoweka baada ya kuzingirwa na maji ya mto Mapogoro yaliyobadili mkondo wake.

Katika mazingira ya kushangaza baadhi ya kaya 83 zinazoishi kitongojini hapo zimekataa kuhama katika eneo hilo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela aliyefika katika eneo hilo juzi kujionea hali halisi zikidai kwamba zitafanya kila ziwezalo kudhibiti mafuriko hayo.

Akiwa na baadhi ya wanahabari, Kasesela na msafara wake walilalazimika kuvua viatu kabla kuvushwa kwa msaada wa askari Polisi na wananchi wengine hadi katika kitongoji hicho kupitia mkondo mpya mkubwa wa maji uliozingira kaya hizo.

Baada ya kujionea hali hiyo mkuu wa wilaya huyo alizimbia kaya hizo kwamba zipo katika hatari ya kuendelea kuathiriwa na mafuriko hayo ikiwa ni pamoja na kupoteza maisha yao endapo hazitahama eneo hilo ambalo baadhi ya nyumba zake zimebomoka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha, huku ardhi yake ikiendelea kumegwa na mkondo wa maji ya mto Mapogoro yaliyochepuka.

“Hali hii ni hatari sana na kwa kweli tunahitaji nguvu ya ziada ya kuzuia maafa haya, nyumba zinaendelea kubomoka, mashamba yanaharibiwa na hata miundombinu mingine kama nguzo za umeme ipo hatarini kung’olewa,” Kasesela alisema huku akiwasihi wananchi hao kuhamia katika eneo lililotengwa.

Alisema kwa upande wake serikali itafanya kila iwezelo kutekeleza jukumu lake la msingi la kuwapatia makazi ya muda wananchi hao na kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha wanapata mahitaji mengine ya msingi.

Afisa Tarafa ya Idodi, Ayubu Kiwanga alisema wananchi hao wanatakiwa kuhamia kwenye eneo maalumu lililotengwa katika kijiji cha Mapogoro ambako pia watapewa maeneo ya kujenga makazi yao ya kudumu.


author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top