Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MUENDELEZO WA HABARI: AGIZO LA RAIS MAGUFULI LAANZA KUTEKELEZWA WAZIRI MAHIGA ARUDISHA FOMU

Baada ya waziri mkuu kutaja majina ya mawaziri wanne na naibu waziri mmoja ambao hawajarudhisha fomu za Sekretariati ya maadili ya umma na kutakiwa wawe wamerejesha fomu hizo mpaka saa kumi na mbili jioni ijumaa ya leo mpaka sasa ni waziri mmoja aliyetii agizo hilo

Aliyerudisha fomu hizo ni waziri wa mambo ya nje,ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Mhe.Balozi dkt.Augustine Mahiga ambapo amekiri kuwa ni kweli alikuwa hajarudisha fomu hizo kutokana na majukumu ya kazi yaliyokuwa yamembana
 
ITV pia imefanikiwa kuongea na waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga ambaye naye ametajwa kutorudisha fomu hizo ambapo ameshangaa jina lake likitajwa wakati ameshazirudisha na kwa sasa  ameelekea ofisi za Sektretariati ya maadili kuwasilisha malalamiko yake
 
Pia ITV  naibu waziri wa ofisi ya makamu wa rais,Muungano na Mazingira Mhe.Luhaga Mpina ambapo amesema kuwa atawahisha kurudisha fomu hizo kabla ya saa kumi na mbili jioni.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top