Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

SERIKALI KUFUFUA SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA, YATAKA LIJIENDESHA KIBIASHARA


Serikali imedhamiria kulifufua upya Shirika la Ndege nchini kwa kulinunulia ndege mpya na kulipa mtaji ili lifanye kazi kibiashara na kutengeneza faida kama ilivyokusudiwa awali.
Akizungumza na menejimenti na wafanyakazi wa Shirika hilo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa  amesema kuwekeza kwenye shirika hilo kutaongeza fursa za kiuchumi na kuvutia wasafiri wengi kufika nchini moja kwa moja na kuvutia sekta ya utalii.
Pia waziri Mbarawa amewataka wafanyakazi wa Shirika hilo ambao sio waadilifu na wavivu kuondoka mara moja ili kupisha wafanyakazi wabunifu na wenye mawazo ya kibiashara kuendesha shirika hilo kwa faida.
“Tunataka watu watakaolitoa shirika hili kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa kuliwezesha kiuchumi na kujitegemea ili kushindana na mashirika mengine ya ndege katika biashara“, amesisitiza Mbarawa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATC, Johnson Mfinanga amemwambia Waziri Mbarawa kuwa kwa sasa shirika hilo lipo katika hali mbaya kiuchumi na hivyo kuhitaji nguvu ya Serikali kulikwamua ili litoe huduma inayostahili.

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top