Mchungaji Getrude Rwakatare.
...................
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana juu ya
changamoto ya miji inayokuwa kwa kasi na usimamizi wa sheria za
mazingira, Mkurugenzi wa Nemc, Bonaventure Baya, alisema kigogo mmoja
wa Nemc ambaye amesimamishwa kazi alifanya uamuzi bila kuhusisha baraza
na kushiriki maamuzi ambayo siyo sahihi katika kesi hiyo iliyoendeshwa
kwa muda wa mwaka mmoja.
Alisema Nemc ilipotaka kuchukua hatua dhidi ya nyumba ya Rwakatare
ilipelekwa mahakamani na kesi hiyo iliendeshwa kwa mwaka mmoja, lakini
kigogo huyo akafanya maamuzi mwenyewe na kuficha nyaraka muhimu za kesi,
hali iliyosababisha kufutwa.
“Baada ya kuwasiliana na Mwanasheria Mkuu tumeambiwa baada ya siku
10 utaratibu utakuwa umekamilika na kesi itaanza tena," alisema.
Katika hatua nyingine, Nemc imewatoza faini na kutoa onyo kwa
makanisa, kampuni, taasisi na hoteli ambazo zimekaidi agizo la kuacha
kupiga kelele licha ya wengi kugoma kulipa na kukimbilia mahakamani
kwani sheria inawataka kufanya hivyo.
Aidha, Mkurugenzi huyo wa Nemc aliitaka serikali kuboresha huduma
ya mipango miji ili kudhibiti ujenzi holela, mipango izingatie uwezo wa
kada tofauti za wananchi, 'master plan' zizingatiwe na ihamasishe sekta
binafsi kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu ya kudhibiti taka za aina
zote.
CHANZO:
NIPASHE
Post a Comment