Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea.
............................
Kubenea aliyasema hayo jana kwenye mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba, wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Katika utetezi wake alioanza kuutoa jana, Kubenea alidai kuwa siku
ya tukio, Makonda alimzuia kuzungumza na wananchi waliokuwa wamemwita,
akidai kwamba yeye Rais wa Kinondoni na ameshazungumza, hivyo hakuna
ruhusa ya mtu mwingine kusema.
Akiongozwa na wakili wake, Peter Kibatala, Kubenea alidai:
"Mheshimiwa hakimu, mimi sijatamka maneno hayo kwamba Makonda ni mjinga,
mpumbavu, kibaka na cheo chenyewe cha kupewa bali nilimwambia wewe
umeteuliwa na rais na mimi nimechaguliwa na wananchi… ndipo akaniambia
yeye ni rais wa Kinondoni akishaongea hakuna ruhusa ya mtu mwingine
kuongea."
Kubenea alidai kuwa Desemba 14, 2015 katika kiwanda cha TOOKU
Garments Co. Ltd, kilichoko Mabibo External, Ubungo, wakati wa mgomo wa
wafanyakazi wa kiwanda hicho alimwambia mkuu huyo wa wilaya kwamba
hawezi kufunga mkutano bila yeye mbunge kuzungumza kwa sababu ni
mwakilishi wa wananchi.
“Makonda alinijibu kwamba kila anapozungumza yeye ndiye mtu wa
mwisho kwa sababu ni rais wa Kinondoni anachokiamua hakuna kingine”
alidai Kubenea.
Akifafanua zaidi, mshtakiwa alidai kuwa alimweleza Makonda kwamba
yeye ni mbunge na amechaguliwa na wananchi kwa zaidi ya kura 17,000
hivyo ni lazima aheshimu uwapo wake katika tukio hilo.
Alidai pamoja na kujieleza kwamba aliitwa na wananchi kwenye
mkutano huo, DC Makonda hakumpa nafasi ya kuzungumza na badala yake
alimwamuru Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Polisi Magomeni, Denis Mujumba,
kumkamata apelekwe kupumzishwa.
“Kamanda Mujumba alinifuata na kunieleza kwamba niko chini ya
ulinzi. Aliniamuru ninyooshe mikono, nilimhoji ananikamata kwa kosa gani
au kwa kuagizwa na mkuu wa wilaya?” alidai Kubenea.
Pia DC (Mkuu wa Wilaya) Makonda aliamuru raia wa China anayedaiwa kunyanyasa wafanyakazi hao akamatwe na achunguzwe.
Awali, Kubenea alidai mahakamani hapo kuwa siku ya tukio, majira ya
saa tano asubuhi, alifika kwenye kiwanda hicho, baada ya kupata taarifa
za kuwapo kwa mgomo na wakazungumza hadi saa 9.30 jioni.
Alidai akiwa kiwandani hapo alionana na uongozi wa kiwanda hicho,
uongozi wa chama cha wafanyakazi juu ya madai mbalimbali ikiwamo
nyongeza ya mshahara na kwamba wakakubaliana kuongeza asilimia tano toka
Sh 100,000.
Alibainisha kuwa wakiwa bado katika mkutano huo, walisikia ving'ora
na wafanyakazi waliokuwapo nje wakiamini ni Rais Dk. John Magufuli
amekwenda kimbe ni Makonda ameongozana na askari polisi ambao idadi yao
hawezi kuikumbuka.
Kubenea alidai kuwa alitambia uwapo wake, akampa taarifa na mahali
walipofikia na kwamba Mkonda alimweleza kuwa ''Mbunge hawa watu ni
wahuni twende ndani ya kikao tukapambane.
''Tukiwa ndani kikao kilianza upya, muafaka haukupatikana na
Makonda aliahidi kesho yake Desemba 15, 2015 kuwapeleka waziri wa
viwanda na biashara na waziri wa kazi na ajira na akwapa nafasi watu
wengine kuongea yeye akamnyima.
Hatua hiyo imefikiwa baada ya mashahidi watatu wa upande wa
mashtaka ambao ni Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi, ASP Denis
Mujumba (39), Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda pamoja na askari
PC Gabriel kutoa ushahidi wao dhidi ya kesi hiyo inayomkabili Kubenea
na kuufunga.
Katika kesi hiyo, Kubenea anadaiwa kuwa Desemba 14, 2015 katika
kiwanda cha Tooku Garments Co.Ltd kilichopo Mabibo External alimtolea
lugha ya matusi DC Makonda kuwa wewe ni kibaka, mjinga, mpumbavu tena
umeteuliwa kwa kupewa.
CHANZO:
NIPASHE
Post a Comment