Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

UEFA CL DRAW : MAN CITY, MAN UTD, SPURS NA LIVERPOOL KUJUA NANI WATAKABILIANA NAO LEO

Manchester City, Manchester United, Tottenham na  Liverpool leo zitajua timu watakazo kabiliana nazo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa  Ulaya katika hatua ya makundi yatakayopangwa leo jioni Alhamisi.
Makundi hayo yatapangwa leo Alhamisi katika mji wa Monaco.
Kumepangwa kuwa na makapu manne yenye timu nane, ambapo kila timu kutoka kila kapu itaunda Kundi,lakini kwa timu zinazotoka nchi moja haziwezi kuwa kundi moja. 
Mabingwa wa EPL Man City,waliotolewa na Liverpool katika hatua ya robo fainali msimu uliopita, wako kapu la kwanza na mabingwa watetezi Real Madrid, Mabingwa wa Europa Ligi Atletico Madrid, Barcelona, Bayern Munich, Juventus, Paris Saint-Germain na  Lokomotiv Moscow.
Man United na  Spurs, waliotolewa kwenye hatua ya 16 bora msimu wa 2017/2018,wako kapu la pili,lenye timu za Borussia Dortmund, Porto, Shakhtar Donetsk, Benfica, Napoli na Roma.
Kikosi cha Jurgen Klopp’s Liverpool watakuwa kapu la tatu na Schalke, Lyon, Monaco, Ajax, CSKA Moscow, Valencia na  PSV Eindhoven.
Mabingwa nchini Serbian  Red Star, bingwa  1991, atakuwa  Viktoria Plzen, Club Brugge, Galatasaray, Young Boys, Inter Milan, Hoffenheim na  AEK Athens.
Mechi za mwanzo za makundi zitaanza kati ya  Septemba 18 na 19, huku fainali itapigwa katika uwanja wa nyumban wa Atletico Madrid’s Wanda Metropolitano Stadium mnamo  June 1.
Na Chediel Charles
CHANZO:Vyombo vya habari vya kaimtaifa.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top