Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KAGAME CUP 2012:AZAM YATANGULIA FAINALI,NANI WA KUMFUATA KATI YA YANGA VS APR

Michuano ya Kombe la Kagame leo inaingia katika hatua ya nusu fainali huku wenyeji Tanzania ikiwakilisha na kwabu mbili za Yanga na Azam Fc.

Katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali timu ya Azam FC itaumana na Vita Club kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.




Kikosi cha Azam Fc leo kinashuka katika Mchezo wa Kwanza wa nusu Fainali Kagame Cup 2012 kwa kupambana na Vita Club ya Jamhuri ya kiDemokrasia ya Congo.
Azam FC Vs AS Vita, Nusu Fainali Kagame Cup, Wanaoanza leo ni
1. Deogratius Munishi GK (27)
2. Ibrahim Shikanda (21)
3. Erasto Nyoni (6)
4. Aggrey Morris (13) Captain
5. Said Moradi (15)
6. Jabir Aziz (25)
7. Kipre Tchetche (10)
8. Ibrahim Mwaipopo (4)
9. John Bocco(19)
10. Salum Abubakar (8)
11. Ramadhan Chombo (17)

Wakati katika mchezo wa pili mabingwa watetezi wa Kombe hilo timu ya Yanga itashuka dimbani kutafuta nafasi ya kucheza fainali itakapo pambana na timu ya APR ya Rwanda.

Mwaka jana Yanga ilitwaa ubingwa wa michuano hiyo inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) baada ya kuwafunga mahasimu wao timu ya Simba kwa bao 1-0.

Mabingwa watetezi Yanga ambao leo katika mchezo unaotazamiwa kuanza saa kumi watarusha karata zao watakapochuana na APR ya Rwanda katika mchezo unaotazamiwa kuwa wa kukata na shoka.

.............................................

Tunawatakia kila la kheri wawakilishi hao wa Tanzania katika michezo yao Leo


...................................................

UPDATE;AZAM VS VITA

DK 35: AZAM 0 - 1 AS VITA (kafunga Alfred

Dk ya 60 VITA CLUB 1 AZAM 0 RED Card kwa mchezaji Vita

AZAM 1 VITA 1 Dk 68 ( Bocco)

Kipindi cha pili chaanza, Mshambuliaji John Boko awainua mashabiki wa Azam FC na Watanzania kwa kusawazisha bao.Mpira unaendelea

DK 89: Azam Fc 2 (Mrisho Ngassa)- 1 As Vita

Mrisho Ngasa awainua tena mashabiki wa Azam na Watanzania kwa kupachika bao la pili dhidi ya AS Vita.(2-1)

FT: Azam FC 2-1 Vita

Mpira Umekwisha Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Azam yaichapa As Vita 2-1

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top