Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KUTOKA BUNGENI:Lukuvi na Werema waomba Spika kutoa sehemu ya hotuba ya inayoelezea "mauaji ya kisiasa" ni katika hotuba ya Kambi ya Upinzani




HOTUBA YA MSEMAJIMKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHESHIMIWA VINCENT JOSEPHAT NYERERE (MB), KUHUSUMAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013 WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Imezuiwa kwa muda kusomwa bungeni ili iweze kujadiliwa kwani kwa mujibu wa Spika imegusia Kesi ambazo ziko mahakamani.

Lakini Mh.Tundu Lissu anasema:Tumetaja masuala ya vifo vya kisiasa na si masuala yaliyopo mahakamani!Wataje kesi namba,wahusika

Akadakia Mh.Lukuvi:All issues found in pg3-5 touches matter in court.They have to be removed first before submission.

Nae Mwanasheria Mkuu akiongezea ...
AG,Werema:Chief whip wa Opp.anaongoza kwa kutokuwa na nidhamu.Na ushahidi amevunja sehemu ya meza yake.

Na Kesi zinazoongelewa ni Kesi zilizopo Katika hotuba ya Waziri Kivuli,V.Nyerere ambazo zisisomwe; 1.Dr.Ulimboka 2.Mch.Msigwa 3.Highness(MB):kujeruhiwa.


Alipopewa nafasi aongee Mh.Cheyo alisema:Tunaomba watu watoe hoja kwa utulivu bila hata kuvunja madeski.

Ndipo Spika akatoa maagizo..
Mh.Makinda:Sehemu ya mauaji ya kisiasa yarukwe!Tutaenda kufatilia.Tukirudi kama haina shida utawasilisha.Ruka mpaka uk.7

Makinda:Nimeshaamua.Aruke,na aendelee uk.7!Kamati ya maadili itapitia uk 3-6 na kujiridhisha kama yanaweza kusomwa Bungeni.

Baada ya Maagizo hayo ya Spika ,Mh.Lissu ameomba muongozo...
Lissu: Muongozo; Kwanini watoa hoja wengine wakitoa hoja hawakatishwi ila wa upande wa wachache wanakatishwa na kuzuiwa kusema?





author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top