Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

HUKU SHIRIKA LA UDA LIKITUSHINDA WENZETU CHINA BADO WANAENDESHA MASHIRIKA YAO MPAKA SASA LIKIWEMO LA TAXI




 
Wakati serikali ya Tanzania imeshindwa kusimamia mashirika ya umma na badala yake kuyabinafisisha, China bado inasimamia na kuendesha huduma nyingi na kwa ufanisi wa hali ya juu. Picha hizi ni mfano tu wa shirika la Taxi Mjini Harbin, China. Hii ni kampuni ya serikali ya mji wa Harbin na kwa huu mji ina idadi ya Taxi zinazofikia 1,200. Hapa zinavyoonekana kwenye picha, ni wafanyakazi wako kwenye kikao. Tanzania inabidi tujifunze. Mabasi ya abiria pia yanamilikiwa na kusimamiwa na serikali, ukiachana na huduma zingine nyiingi. Tanzania tungeweza kubadilika na serikali ikaweza kusimamia huduma za msingi ingekua chachu ya maendeleo. Vinginevyo serikali iwe na uwezo wa kutoa tenda ila si kwa asilimia 10 kwani asilimia kumi ndo inayofanya ufanisi usiwepo, pamoja na kupeana tenda kindugu au kirafiki.
Ubinafsishaji  wa Shirika la Usafirishaji Dar es Salaam (UDA) ambao ulizua malumbano kutokana na kugubikwa kwa rushwa hii ikiwa tofauti na wenzetu China ambao wana mpaka mashirika ya Taxi.

Tuna ya kujifunza kupitia nchi zingine zilizotuacha kimaendeleo na tujue hata siku moja maendeleo hayaji kama muujiza.
..........................................
Kutoka China na Zeph
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top