Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

WASIWASI WARUDI PIBOR,SUDANI KUSINI

Kuna mvutano na wiwasi katika mji wa Pibor, Sudan Kusini, karibu na mpaka wa Ethiopia.
Ghasia za Sudan Kusini zinatokea mara kwa mara
Shirika la kimataifa la msaada wa matibabu, MSF, limewaondosha wafanyakazi wake wa kigeni na wengi walio wenyeji wamekimbilia vichakani.

Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Sudan Kusini, Hilde Johnson, amesema hali katika mji wa Pibor ni ya wasiwasi, na kuna ripoti kuwa wakaazi wamekimbilia vichakani.

Kuondoshwa kwa wafanyakazi wa MSF kumewaacha watu kama 90,000 bila ya huduma za afya.

Tisho linatokana na kiongozi wa wapiganaji, David Yauyau, ambaye amewavutia vijana wa kabila la Murle.

Inaarifiwa kuwa wenyeji wamekerwa na wanajeshi wa serikali ya Sudan Kusini waliowekwa kwenye eneo hilo, wengi wao kutoka kabila la maadui wao la Nur.
Inasemekana wanajeshi hao wamewapiga na kuwabaka baadhi ya wenyeji.

Umoja wa Mataifa unasema unafuatilia hali hiyo kwa makini na uko tayari kutuma askari zaidi kujumuika na kikosi cha kusimamia usalama kilioko mjini Pibor chenye askari 80.

Mwaka jana maelfu ya watu wa kabila la Nur waliwashambulia Wamurle huko Pibor na kuuwa watu kama 150.

Mapigano kuhusu ng'ombe na wanawake yanatokea mara kwa mara Sudan Kusini.

Via BBC Swahili
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top