Na Katuma Masamba
Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora nchini bado inafanyia kazi malalamiko yaliyowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la
Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) anayetaka kujua kiini cha wakazi wa Goba
kutokupata maji.
Mnyika aliwasilisha
barua yake yenye malalamiko kwenye Tume hiyo ili kujua tatizo linalosababisha kata
ya Goba kukosa huduma ya maji tangu mwaka 2007.
Mkurugenzi wa Tume
hiyo ya Haki za Binadamu na Utawala
Bora, Francis Nzuki alisema malalamiko hayo bado wanayafanyia uchunguzi ili
kubaini tatizo linalofanya kata hiyo isipate maji kwa muda mrefu sasa.
Alisema baada ya
kukamilika kwa uchunguzi watatoa majibu haraka iwezekanavyo juu ya malalamiko
hayo ila kwa sasa bado wanaendelea kufanyia kazi malalamiko hayo.
Wakazi wa Goba
wanalalamikia ukosefu wa maji unaowaathiri wakazi kwa muda mrefu sasa ambapo
hulazimika kununua ndoo moja yenye ujazo ya lita 20 kwa Sh 500 hadi Sh 700.
Naye Mnyika alisema
amekuwa akijitahidi kufanya juhudi ili wapiga kura wake waondokane na tatizo
hilo na kuongeza kwamba Halmashauri ya Kinondoni ndiyo inayokwamisha kata hiyo
isipate maji.
Mnyika alisema
anaendelea kusubiri taarifa itakayokuwa na majibu ya malalamiko yake ili ajue
tatizo liko wapi kwa wananchi kukosa maji miaka yote hiyo.
Post a Comment