Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

LOWASSA AZUNGUMZIA TUME YAKE

Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ameitwisha zigo serikali na kusema kwamba katika uongozi wake tume ya watalaam iliyoundwa kuchunguza maghorofa yanayojengwa chini ya viwango hapa nchini mwaka 2006, ilimaliza kazi yake na kuwasilisha ripoti katika ofisi ya Waziri Mkuu.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam ambao walitaka kupata maoni yake kuhusu tume aliyounda kuchunguza maghorofa mbalimbali yanayojengwa chini ya viwango hususani jijini Dar es Salaam, Lowassa alisema yeye alimaliza  kazi yake na kwamba ripoti hiyo imekaliwa na ofisi ya Waziri Mkuu.
 
Hata hivyo, Lowassa hakutaka kuingia kwa undani katika suala hilo kwa madai kwamba ofisi ya Waziri Mkuu ina taarifa zote ambazo zimo katika ripoti ya mwaka 2006.
 
“Nendeni mkaulize ofisi ya waziri mkuu mimi sipo huko na ripoti hiyo ya watalaam ipo katika ofisi ya waziri mkuu mimi sina cha kusema,” alisema Lowassa.
 
Ripoti ya tume hiyo iliyojulikana kama "tume ya Lowassa" ilibaini maghorofa 100 jijini Dar es Salaam yalitakiwa kubomolewa kutokana na kubainika kuwa na kasoro za kitalaam jambo ambalo hadi sasa halijafanyika.
 
Msemaji wa ofisi ya ofisi ya waziri alipotafutwa jana ofisini kwake kuzungumzia ripoti hiyo ya watalaam hakupatikana na NIPASHE iliambiwa kuwa yupo nje ya ofisi kikazi.
 
Wiki iliyopita jengo la ghorofa 16 liliporomoka na kuua watu 30 na wengine kujeruhiwa huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni kutokana na kujengwa chini ya viwango vinavyotakiwa.
 
Tayari serikali imeunda tume nyingine inayoongozwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi kuchunguza ajali hiyo.
 
CHANZO: NIPASHE
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top