Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CESC FABREGAS AITOLEA NJE MAN U ASEMA ANATAKA KUBAKI BARCELONA

KOCHA wa Manchester United, David Moyes amepata pigo lingine baada ya kiungo wa Barcelona, Cesc Fabregas kumuambia kocha wake, Tito Vilanova anataka kubaki kwa vigogo hao wa Katalunya ili kuweza kupata mataji zaidi.
 
United ilithibitisha kutenga dau la Pauni Milioni 26 kwa ajili ya Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal ili kuweza kuungana na RVP ambao waliwahi kucheza pamoja.
 
Harakati hizo zilikuja baada ya Thiago Alcantara kuamua kujiunga na kocha wake wa zamani, Pep Guardiola katika klabu ya Bayern Munich badala ya mabingwa hao wa England. 
 
Na sasa kocha wa Barca, Vilanova ameanza mazungumzo na Fabregas ambaye ameweka wazi anataka kubaki Nou Camp.
 
Vilanova alisema: "Cesc amepata ofa kutoka klabu nyingine. Nimezungumza naye na ameniambia anataka kubaki. Ndoto zake ni kung'ara akiwa hapa ''
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top