Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

''NDOO ZA RANGI HATARI KIAFYA''

na Betty Kangonga


WATANZANIA wametakiwa kuepuka matumizi ya ndoo zinazohifadhiwa rangi kwa ajili ya kuhifadhia maji ya kunywa kutokana na ndoo hizo kuwa na athari kiafya.
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Mhadhiri Mshauri wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili (MUHAS), Dk. Vera Ngowi, alisema kuwa ukosefu wa elimu ya athari ya viuatilifu imekuwa chanzo cha jamii kushindwa kubaini athari zinazoweza kuwapata.
Dk. Ngowi alisema ndoo hizo si salama kwa matumizi kutokana na rangi kuwa na kemikali zinazoweza kusababisha magonjwa mbalimbali ikiwamo saratani.
Alisema ni muhimu viwanda vinavyozalisha bidhaa hiyo vikaweka tahadhari ili jamii iepuke kutumia ndoo hizo kwa ajili ya kuhifadhia maji.
“Hivi sasa baadhi ya Watanzania wanapenda kutumia ndoo hizo kwa ajili ya kuhifadhia maji, lakini napenda kuwaasa waepuke matumizi ya vifaa hivyo kwa kuwa vinaweza kusababisha magonjwa ya ngozi na hata saratani,” alisema.
Alisema watengenezaji wa bidhaa mbalimbali walio wengi wanashindwa kusema ukweli kuhusiana na madhara yanayoweza kupatikana kwa kuwa wanahofia kupata hasara.

CHANZO:Tanzania Daima
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top