Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TASWIRA KUTOKA IRINGA WAFANYABIASHARA WAGOMEA MASHINE ZA EFD,WAFUNGA MADUKA

wafanyabiashara  Iringa  wakiwa katika mgomo  eneo ya Miyomboni  leo 
Maduka  Miyomboni  yakiwa  yamefungwa  leo 
Wateja  wakiwa  wamekwama  kupata huduma  le 
Maduka  mbali mbali ya mjini Iringa yakiwa yamefungwa leo 
Wafanyabiashara  eneo la stendi ya  Miyomboni  wakiwa  wamesimama nje ya maduka yao leo 

Mfanyabiashara  Erick Makofia  akipita  eneo la Miyomboni leo  ...................................................................................................
 HALI  ya  swari  katika  mji  wa Iringa kufuatia  kuanza kwa mgomo  usio na kikomo wa wafanyabiashara kama njia ya  kufikisha ujumbe  kwa  waziri wa fedha  na  serikali ya  Rais Jakaya  Kikwete  juu ya gharama za mashine za EFD

Mgomo huu umeanza leo  asubuhi  hii katika mjini  wa Iringa  huku  wakipanga kufanya maandamano  kuwaadhibu wenzao wanaokiuka mgomo huo.
Hali kwa upande wa wakazi wa Iringa mjini  na wale wa maeneo na wilaya  na mji mingine wanao kuja kwaajili ya kupata huduma imewapa wakati mgumu kutokana na mgomo huo, hivyo kujikuta wakiambulia makufuri katika maduka
Hata  hivyo  wafanyabiashara  hao  wametoa onyo kwa  wenzao  iwapo  watafungua  maduka yao  watakiona cha moto  na  kuwa  kuanzia  wakati  wowote sasa  wataanza msako wa duka moja hadi jingine kwani amesema mgomo  huo ni nchi  nzima na wao  wametii uamuzi wa  wafanyabiashara  wa jijini Dar es Salaam ambao  pia  wapo katika mgomo kama  huo 

Mkuu wa mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma  amewaangukia wafanyabiashara  hao kwa kuwataka   kutoaendelea na mgomo  huo  bali kuendelea na biashara  hata kama bila mashine  hizo  wakati serikali ikitafuta  suluhu  ya  suala  hilo.
Akizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com kwa njia ya simu Dr Ishengoma  alisema kuwa  si busara kwa  wafanyabiashara hao  kugoma kwani toka  awali si wote walikuwa na mashine  hizo na bado waliendelea kufanya shughuli zao.
" Mbona  siku zote  walikuwa  wanauza bila mashine na hadi sasa hakuna mfanyabiashara  aliyekamatwa kwa kukosa mashine....nawaomba wafungue maduka yao"
Wakati  kamanda wa  polisi  mkoa  wa Iringa Ramadhan Mungi  akiwataka  wafanyabiashara  hao  kutofanya vurugu na kuwa atakayefanya vurugu  jeshi  la polisi  litachukua  hatua kali dhidi  yake na kuwa jeshi hilo limejipanga kwa ulinzi .
 
CHANZO:Mzee wa Matukio Daima.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top