Wanafunzi
wakilazimika kutembea kwa miguu kuelekea shuleni kutokana na mgomo wa daladala maarufu kama 'vifodi' ulioingia siku ya pili leo kwa baadhi ya njia.
Wananchi wakitumia gari za mizigo ili kuwahi makazini kutokana na mgomo wa vifodi ulioanza jana na kuingia siku ya pili leo .
Kile kinachotafsiriwa kuwa mgomo wa waendesha magari madogo ya kubeba abiria kwa Jiji la Arusha maarufu kama “vifodi” umeendelea tena hii leo ikiwa ni siku ya pili mfululizo kwa baadhi ya njia.
Kwa mfano kwa njia ya kutoka maeneo ya Moshono kuelekea mjini hakuna gari yeyete ya abiria kabisa, halikadhalika njia itokayo Njiro kwenye mjini pia.
Wasafiri wa njia hizo wamejikuta wakilazimika kusafiri katika mazingira ya hatari kwa kujazana kwenye magari ya wazi na pikipiki za mizigo vyombo ambavyo si maalumu kwa ubebeaji wa abiria.
Uchunguzi wa Blog hii umegundua kuwa wanaosababisha zaidi hali hii ni wapiga debe ambao wanaona kwa mfumo mpya wa hizi njia za usafiri kama mpango wa Jiji kukabiliana na msongamano barabarani hawataweza kupata ujira wa kuitia abiria kwenye magari, na hivyo baadhi yao kuwafanyia vurugu madereva wanaotaka kufanya kazi.
Lakini pia kuna baadhi ya madereva ambao ni kama hawauelewa utaratibu huo mpya na kujikuta wakigoma kuendesha magari yao.
Habari kwa hisani ya Arusha255
Post a Comment