Masaibu ya Jose
Mourinho msimu huu yaliendelea baada ya vijana wake kubanduliwa kutoka
shindano la League Cup na Stoke City kupitia mikwaju ya penalti mechi
iliyochezwa Jumanne usiku.
Arsenal pia hawakuwa na bahati kwani walitupwa nje baada ya kuchapwa 3-0 na Sheffield Wednesday.
Arsenal,
waliofanya mabadiliko saba kwenye timu iliyolaza Everton 2-1 Jumamosi,
walipata matatizo zaidi kwani Theo Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain
waliondoka uwanjani baada ya kuumia dakika 20 za kwanza. Mechi yote
walikuwa na makombora mawili pekee yaliyolenga goli.
Uwanja wa
Brittania, baada ya Chelsea kudhibiti mpira kipindi cha kwanza ambacho
hakikuzaa bao lolote, Stoke walitwaa uongozi kupitia Jon Walters dakika
ya 52.
Loic Remy aliwaokoa Chelsea, japo kwa muda alipofunga bao
dakika ya 90, sekunde chache kabla ya mchezaji wa Stoke Phil Bardsley
kufukuzwa uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.
Stoke
walifunga mikwaju yao yote, lakini Eden Hazard akakosa mkwaju wake
uliokuwa wa mwisho, ambao ulizimwa na kipa Jack Butland.
Mashabiki waStoke walifurahia sana masaibu ya Mourinho na kumcheka, wengine wakisema huenda akafutwa Jumatano asubuhi.
Chelsea
walilazwa 2-1 na West Ham Jumamosi katika mechi ambayo Mourinho
alifukuzwa eneo wanamokaa makocha baada yake kumtafuta na kumzungumzia
refa Jon Moss wakati wa mapumziko.
CHANZO:BBC SWAHILI
Post a Comment