Kila
siku watafiti wana habari mpya kuhusiana na maisha, tumeona tafiti
nyingi zikifanywa zikiwemo za magari, majumba, watu maarufu.. Lakini
sikuwahi kufikiri kwamba kuna siku nitakutana na utafiti unaozungumzia
urefu wa Marais duniani.
1. Filip Vujanovic
Papa Benedict xvi akiwa na Rais wa Montenegro ambaye ndiye rais mrefu kuliko wote duniani, ana urefu wa futi 6.5
2.Nicolas Maduro
Huyu ni Rais wa Venezuela, anashika nafasi ya pili kwa kuwa rais mrefu, ana urefu wa futi 6.3
3.Bashar Al- Assad
Huyu ndiye Rais wa tatu kwa urefu duniani kutoka Syria, ana urefu wa futi 6.2
4.Stephen Harper
Huyu ni Waziri mkuu wa Canada, ana urefu wa futi 6.2
5. Toomas Hendrik Ilves
Huyu ni rais wa Estonia ambaye pia aliwahi kuwa mwandishi wa habari, ana urefu wa futi 6.2
6. Paul Kagame
Kwa
Afrika huyu ndiye rais anayeongoza kwa urefu, lakini duniani anakamata
nafasi ya sita kwa futi 6.2 huku binti yake akimzidi kwa kuwa na futi
6.6. Hapa Rais Kagame alikuwa na Rais Obama na mkewe.
7.Barack Obama
Barack Obama ni Rais wa Marekani, ana urefu wa futi 6.1 huku mke wake Michelle Obama akiwa na futi 5.11
8.David Cameroon
Huyu ni Waziri mkuu wa Uingereza, urefu wake haujatofautiana na wa Rais Obama wa Marekani, wote wana futi 6.1
9.Blaise Compaore
Huyu
alikuwa Rais wa Burkina Faso ambaye Oktoba mwaka jana aliamua kujiuzulu
kutokana na machafuko nchini kwake, ana urefu wa futi 6. Hapa alikuwa
na Rais Obama na wake zao.
10. Recep Tayyip Erdogan
Huyu ni rais wa Uturuki aliyekabidhiwa madaraka mwaka jana, ana urefu wa futi 6
This post was written by: Author Name
Your description comes here!
Get Free Email Updates to your Inbox!
Filed Under:
RAIS OBAMA
on Friday, October 30, 2015
Post a Comment