Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

UKAWA WAKUBALI YAISHE MAENEO YENYE MGOGORO

Tume ya Taiafa ya Uchaguzi (Nec).
Vyama vinne vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimekubali kusimamisha mgombea zaidi ya mmoja kwa ngazi ya udiwani na ubunge katika uchaguzi mkuu ujao ili wananchi wenyewe waamue kupitia masanduku ya kura nani wanayemtaka.

Awali, vyama hivyo vilikubaliana kusimamisha mgombea mmoja kwa kila ngazi kuanzia udiwani, ubunge na urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.

Hata hivyo, kwa nafasi ya urais, vyama hivyo vinne vya NLD, Cuf, Chadema na NCCR-Mageuzi, vimekubaliana kumsimamisha Edward Lowassa.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani kutoka vyama hivyo ambazo zilithibitishwa na Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, vyama hivyo kwa sasa vimekubaliana maeneo ambayo kuna mgombea zaidi ya mmoja ambaye chama chake kipo chini ya Ukawa, wote waendelee kugombea na wananchi ndiyo watakaomua.

Vyama hivyo vilitangaza mgawanyo wa majimbo kabla ya kuanza kampeni za uchaguzi, lakini majimbo 12 hayakupatiwa ufumbuzi wa namna ya kusimamisha wagombea walio chini ya Ukawa.

Kwa mujibu wa Makene, kwa sasa Ukawa haina namna yoyote ya kufanya ili kuweka mambo sawa kwa kuweka mgombea mmoja katika majimbo hayo pamoja na baadhi ya kata ambako kuna zaidi ya mtu mmoja.


Alisema kwa sasa Tume ya Taiafa ya Uchaguzi (Nec), imeishachapisha majina ya wagombea wote katika karatasi za kupigia kura na kwamba hata kama Ukawa watamuondoa mgombea ili kumpisha mwenzake, bado jina lake litaonekana siku ya kupiga kura.

Alifafanua kwamba kwa sasa kumuondoa mgombea kuna hatua ndefu kwani atatakiwa kwenda mahakamani kuapa na kwamba Ukawa imeamua kata na jimbo ambalo kuna mgombea zaidi ya mmoja wabakie hivyo hivyo.

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
Chediel . Powered by Blogger.
© Copyright Rundugai Blog
Back To Top