Rais John Magufuli akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Fedha 
BAADHI ya viongozi wa dini na jamii kwa ujumla wamemtaka Rais 
wa awamu ya tano, Dk. John Magufuli kuhakikisha anampata Waziri Mkuu 
mchapa kazi na si vinginevyo. Anaandika Dany Tibason, Dodoma … 
Waliyasema hayo kwa vile wanaamini Waziri Mkuu ndiyo msimamizi mkuu wa mambo yote ya serikali, hivyo kukosea kwake kunaweza kukamfanya akashindwa kutekeleza ahadi zake.
Askofu wa Kanisa la Methodist jimbo la Dodoma, Joseph Bundara, 
amesema ili nchi iweze kusonga mbele ni lazima apatikane waziri mkuu 
mwenye kusimamia maamuzi yasiyotetereka.
“Kwa sasa taifa letu wananchi wake wana hali mbaya kiuchumi hivyo 
wanakabiliwa na umasikini wa kutupwa huku kundi la watu wadchache 
wakijineemesha.
“Ili kuondoa hilo waziri mkuu ambaye ni msimamizi mkuu wa serikali 
anatakiwa kuhakikisha anasimamia misingi ya utawara bora ikiwa ni 
kuhakikisha rasilimali za nchi zinatumiwa vizuri na kuwanufaisha 
wananchi wote,” amesema Askofu Bundara.
Mbali na hilo alimtaka Rais Dk. Magufuli kuhakikisha anasitisha 
matumizi mabaya ya rasilimali za serikali ambayo kwa hatua kubwa 
yamesababisha nchi kuyumba na kuwafanya watanzania kuwa masikini.
Naye Hawa Makau, ambaye ni mkazi wilayani Mpwapwa, amesema ili taifa 
liweze kusonga mbele ni lazima baraza la mawaziri liwe dogo na lenye 
tija.
Aidha amesema rais huyo wa awamu ya tano anatakiwa kuwachagua 
mawaziri na manaibu ambao ni wachapa kazi na asiangalie ukanda wala 
kutoa nafasi hizo kwa upendeleo.
“Taifa hili lina watu wengi wasomi na wenye uwezo mkubwa wa kufanya 
kazi lakini mara nyingi hawapewi nafasi hizo kwa sababu ya viongozi wa 
juu kulindana na kubebabana na wakati nafasi hizo upeana watoto wa 
wakubwa.
“Nafasi za uongozi zitolewe kwa kuzingia ujuzi na uelewa wa mtu na 
isiwe fadhila au kutomteua mtu mwenye uwezo kwa sasabu binafsi za 
chuki,” alieleza Makua.
Licha ya uteuzi wa Mawaziri na Manaibu wake pia Makau alizungumzia 
kuhusu suala la uteuzi wa wakuu wa wilaya na mikoa kuwa nao ulenge kwa 
vijana ambao wametoka vyuoni wenye taaluma badala ya kuendelea na 
waliopo kwa sasa ambao hata wao wanaonekana kushindwa kazi.
“Mimi najiuliza maswali mengi ni kwanini wakuu wa wilaya na wakuu wa 
mikoa wanachaguliwa hao hao tu wakati wapo vijana wengi wasomi na wenye 
uwezo mkubwa wa kufanya kazi hiyo,” alieleza mwananchi huyo.
SOURCE:MwanaHalisi  
Post a Comment