Siku tatu baada ya kutoka
India alikokwenda kwa ajili ya kupata matibabu, Katibu Mkuu wa Chama Cha
Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad jana alilazwa katika hospitali
ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF
Zanzibar, Nassoro Mazrui amesema kuwa chanzo cha Maalim Seif kulazwa
katika hospitali hiyo jana asubuhi ni uchovu wa safari yake ya India
ambayo alienda kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa mgongo.
Mazrui alikanusha taarifa
zilizokuwa zinaenezwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kiongozi huyo wa
CUF alilazwa kutokana na matatizo ya moyo. Alisema kuwa hakuna
kumbukumbu yoyote ya ripoti ya daktari inayoonesha kuwa Maalim Seif ana
tatizo la moyo.
Naibu Katibu Mkuu huyo wa
CUF alisema kuwa kiongozi huyo anaendelea vizuri kiafya na kwamba hayuko
katika hali mahututi kama ilivyokuwa ikielezwa.
“Anakula na kufanya kila
kitu mwenyewe na hata jioni hii nimeongea naye, anakula kila kitu, hivyo
Watanzania wasiwe na wasiwasi juu ya afya ya Maalim Seif,” alisema
Mazrui.
Viongozi mbalimbali wa
vyama vya siasa waliwasili katika hospitali hiyo kumjulia hali akiwemo
aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.
MY TAKE: Kwa maoni yangu
Seif Shariff anapaswa kupumzika siasa ili aangalie afya yake kwa sasa
ikiwa ameukosa urais kwa awamu tano ni kheri akapumzika siasa haswa
katika kipindi hiki cha ugonjwa.
Post a Comment